STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 12, 2012

Chelsea, Man City kufungua pazia la msimu mpya EPL leo

PAZIA la msimu mpya wa Ligi Kuu ya England (EPL)kwa mwaka 2012/13 linatarajiwa kufunguliwa rasmi leo Jumapili kwa mechi ya kuwania Ngao ya Jamii kati ya Mabingwa wa Ligi Kuu England, Manchester City, na Mabingwa wa FA Cup, Chelsea, ambao pia ni Mabingwa wa Ulaya. Pambano la timu hizo mbili zitakazoshuka dimbani leo zikiwa na mabadiliko yanayotofautiana katika vikosi vyao unatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa Villa Park, kuanzia saa 9 Alasiri kwa saa za Afrika Mashariki na Kati. Wakati Chelsea ikiwa na nyota wapya walionunuliwa hivi karibuni kwa ajili ya msimu mpya, Man City wao hawana mabadiliko yoyote. Chelsea itashuka dimbani leo ikiwa haina kinara aliyewapa mataji hayo mawili inayoyashikilia kwa sasa Didier Drogba, kutoka Ivory Coast aliyehamia katika klabu ya Shanghai Shenhua ya China akiungana na Nicolas Anelka. Vifaa vipya vilivyosajiliwa na ambavyo vimeanza kuonyesha makeke katika mechi za kujipima nguvu kujiandaa na msimu mpya utakaoanza mwishoni mwa wiki ijayo ni Eden Hazard, Marko Marin na Oscar lakini ni Hazard na Marin ambao wanaweza kucheza Mechi hii na Man City kwa vile Oscar atakuwa bado yuko na nchi yake Brazil kwenye Olimpiki. Msimu uliopita, Timu hizi ziligawana ushindi kwa Chelsea kuifunga Man City 2-1 Mwezi Desemba na Man City kuifunga Chelsea 2-1 Mwezi Machi. Katika Mechi zao za hivi karibuni, Mechi za kujipasha kwa ajili ya Msimu mpya, Chelsea imekuwa na matokeo yasiyoridhisha kwa kushinda Mechi moja tu kati ya 4 walizocheza na kufungwa zilizobaki wakati Man City wamecheza Mechi 5 na kushinda 3 na kufungwa mbili. Chelsea hawana majeruhi yeyote lakini Man City watamkosa Nahodha wao Vincent Kompany na Micah Richards ambao wameumia. Vikosi vinatarajiwa kupangwa kwa siku ya leo ni kama ifuatavyo: Chelsea [Mfumo 4-3-3]: Cech, Ivanovic, Terry, Cahill, Cole, Mikel, Meireles, Lampard, Ramires, Torres, Hazard Man City [Mfumo 4-4-2]: Hart, Zabaleta, Savic, Lescott, Clichy, Yaya Toure, De Jong, Nasri, Johnson, Tevez, Aguero

No comments:

Post a Comment