STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 11, 2012

Vazi la taifa miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika

Waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo Dk Fenella Mukangara

VAZI rasmi la Taifa linatarajia kuanza kuvaliwa siku ya kilele cha sherehe za miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania zitakazofanyika Desemba 9, mwaka huu imeelezwa.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alisema vazi hilo litavaliwa baada ya mchakato mzima wa kulipata vazi hilo utakapokamilika ambapo umepitia hatua mbalimbali.
Waziri Fenella alisema wizara yake inatarajia kuchukua michoro minne kati ya tisa iliyopitishwa na Kamati ya Vazi la Taifa iliyoundwa ambapo pia mchakato huo unahusisha kupata aina ya kitambaa kitakachotumika kutengenezea vazi hilo.
Waziri huyo alisema kuwa michoro hiyo minne (miwili ya vazi la kitenge na mingine ya khanga) itachukuliwa na kuwasilisha kwa sekretariati ya Baraza la Mawaziri ambalo litatakiwa kufanya maamuzi kabla ya Oktoba 31 mwaka huu.
"Baada ya kupata vazi hilo,kila mtu atakuwa na uhuru wa kuvaa mtandio, kushona gauni, shati au kuvaa kitambaa cha kichwani ambacho kitakuwa kinaonyesha vazi la taifa," alisema Fenella.
Katibu wa Kamati ya Vazi la Taifa, Angella Ngowi alisema kuwa kamati yake ilipokea maoni kutoka katika sehemu mbalimbali nchini na kuongeza kwamba mchakato wa kupata vazi hilo ulianza mwaka 2003.
Alisema kuwa michoro yote iliyopo katika mchakato huo ina rangi za bendera ya taifa na alama mbalimbali kama picha ya mlima Kilimanjaro, mwenge wa Uhuru, ala za muziki na picha za wanyama (Twiga na Pundamilia).


No comments:

Post a Comment