STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 10, 2012

Miyeyusho, mtwanga Nassib na kutwa taji la WBF






Bondia Fransic Miyeyusho akionesha ufundi wake kwa kumtupia masumbwi Nassibu Ramadhani wakati wa Mpambano wao wa kugombania ubingwa wa WBF uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Miyeyusho alishinda kwa T.K.O ya raundi ya kumi picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Mohamed Matumla  kulia  akimuhadhibi Doi Miyeyusho wakati wa mpambano huo usiku wa kuamkia  leo Matumla alishinda kwa K,O raundi ya pili Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Juma Fundi kushoto na Fadhili Majia wakioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki Majia alishinda kwa pointiPicha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Miyeyusho kushoto akimwazibu mpinzani wake Nassibu Ramadhani kwa kumtupia makonde mazito wakati wa Mpambano wao wa kugombania ubingwa wa WBF uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Miyeyusho alishinda kwa T.K.O ya raundi ya kumi picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Miyeyusho akionesha ufundi wake kwa kumtupia masumbwi Nassibu Ramadhani wakati wa Mpambano wao wa kugombania ubingwa wa WBF uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Miyeyusho alishinda kwa T.K.O ya raundi ya kumi picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mkangara kulia akimvisha mkanda wa ubingwa wa WBF bondia Fransic Miyeyusho baada ya kumtwanga Nassibu Ramadhani  kwa T.K.O raundi ya kumi kushoto ni promota wa mpambano huo Mohamed Bawaziri www.superdboxingcoach.blogspot.com
Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mkangara kulia akimpongeza Bingwa wa ubingwa wa WBF bondia Fransic Miyeyusho baada ya kumtwanga Nassibu Ramadhani  kwa T.K.O raundi ya kumi kushoto ni promota wa mpambano huo Mohamed Bawaziri www.superdboxingcoach.blogspot.com
bondia Fransic Miyeyusho akiwa amebebwa juu akiwa na mikanda miwili alioshinda baada ya kumtwanga Nassibu Ramadhani picha nwww.superdboxingcoach.blogspot.coma
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila  'Super D' kushoto akiwa na wadau waliojitokeza kuangalia mpambano huo
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Francis Miyeyusho juzi alifanikiwa kutetea taji lake la Mabara la UBO na kunyakua taji jipya pia la Mabara la WBF baada ya kumtwanga kwa TKO 10 mpinzani wake Nassib Ramadhani.
Miyeyusho alimtwanga Nassib TKO hiyo katika raundi ya 10 katika pambano kali lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam na ikuhudhuriwa na viongozi na wanamasumbwi mbalimbali nyota nchini.
Pambano hilo lililoandaliwa na mratibu Mohammed Bawazir na lililokuwa la kwanza kwa mabondia hao lilikuwa na jumla ya raundi 12 uzito wa bantam na lilianza kwa Nassib kumpeleka puta mpinzani wake kwa makonde makali.
Hata hivyo kadri raundi zilivyokuwa zikisonga mbele Nassib alianza kuonekana kuishiwa pumzi hasa kuanzia raundi ya nane na kumpa nafasi mpinzani wake nafasi ya kusimama imara kabla ya kusalimu amri katika raundi ya 10.
Mara baada ya Miyeyusho kutangazwa kuwa mshindi alikabidhiwa mataji yake mawili na aliyekuwa mgeni ramsi, Waziri wa Habari Utamaduni, Vijana na Michezo Dk Funella Mukangara na kuamsha hoi hoi ukumbini hapo.
Kabla ya pambao hilo, kulikuwa na mapambano mengine ya utangulizi ambapo Mohammed Matumla ' Snake Boy Jr' alimpiga kwa KO Doi Miyeyusho, Deo Samuel alitoka sare na Freddy Sayuni ,Fadhil Majiha alimpiga kwa pointi Juma Fundi na Ibrahim Classic alimpiga kwa pointi Said Mungi.
Baadhi ya mashabiki waliofurika kwenye ukumbi huo waliwapongeza waratibu wa pambano hilo sawia na kuwasifu mabondia wote waliopigana siku hiyo husuisani kumwagia sifa Nassib wakidai ni 'bonge' la bondia licha ya kupoteza mchezo huo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment