STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 21, 2013

Floyd Mayweather kurejea ulingoni Mei $, alamba mkataba mpya

Floyd Mayweather
 
BINGWA wa Dunia wa WBC asioyepigika, bondia Floyd Mayweather ameoata mkataba mnono utakaomwezesha kupigana hadi mara sita ndani ya kipindi cha miezi 30. 
Mkataba huo mnono utamfanya Mayweather kuwa mwanamichezo wa kwanza duniani kuingia mkataba mkubwa kuliko mwana michezo yoyote.
Mkali huyo ambaye anarekodi ya kupigana mapambano 43 akishinda yote, ikiwamo 26 ya kuwapiga wapinzani wake kwa KO, ataanza kuutumikia mkataba huo Mei 4 mwaka huu kwa kuvaana na Robert Guerrero.
Pambano hilo litakuwa la kwanza kwa mkali huyo aliyepanda mara ya mwisho ulingoni Mei 5 mwaka jana na kumtwanga Miguel Cotto kabla ya baadae kupelekwa jela kuitumikia kifungo kwa kosa la kumtwanga mpenziwe.
Mayweather atavaana na Guerrero mwenye rekodi ya kuicheza ,apambano 35, akishinda 31, 18 yakiwa kwa KO, kupigwa moja na kutoka sare moja katika pambano linalosubiriwa kwa hamu kuona kama mkali huyo bado yupo moto au jela imempunguza makali yake.
Katika mkataba wake mpya unahusisha matangazo na kumfanya avune mahela, mbali na mikataba yake mingine iliyomwezesha kuwa mmoja wa wanamichezo wenye noti duniani.

No comments:

Post a Comment