STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 18, 2013

LIVERPOOL YAZINDUKA EPL, YAPIGA MTU 5-0

Steven Gerrard akifunga penati na kuipa uongozi Liverpool jana

LIVERPOOL jana ilizinduka kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kuipa kipigo kitakatifu timu ya Swansea City wa kuifunga mabao 5-0 katika pambano pekee la ligi hiyo lililochezwa jana kwenye uwanja wa Anfield.
Nahiodha Steven Gerrard alianza kuiandikia bao Liverpool katika ya 34 kwa mkwaju wa penati bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Vijana hao wa Brandts Rodgers, kocha aliyekuwa akiinoa Swansea kabla ya kutua Liverpool msimu huu, waliongeza mabao mengine katika kipindi hicho cha pili kupitia Philippe Coutinho aliyefunga dakika ya 46 akimalizia kazi nzuri ya Luis Suarez, kabla ya dakika tano baadaye José Enrique kufunga bao la tatu.
Dakikia ya 56, Suarez alifunga bao la nne na Daniel Sturridge kuhitimisha karamu ya mabao kwa mkwaju wa penati dakika ya 71 na kuifanya Liverpool kupata ushindi wa kwanza katika mechi tano ilizocheza hivi karibuni.
Mechi tatu zilizopita timu hiyo iliambulia sare mbili na kipigo toka kwa West Bromwich, huku pia wakinyukwa katika michuano ya Kombe la Ligi ya Ulaya na Zenith.
Kwa ushindi huo LIverpool imechupa  kutoka nafasi ya tisa hadi ya saba ikiwa na pointi 39.

No comments:

Post a Comment