STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 17, 2013

Kila la heri Azam mkisaka heshima Afrika

Kikosi cha Azam

Furaha ya Ushindi: Azam tuypeni raha kama hivi hata mkiwa ughaibuni
WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, Azam jioni ya leo itakuwa ugenini mjini Monrovia, Liberia kusaka heshima barani Afrika ikitarajiwa kuvaana na timu ya maafande ya Barrack YC II katika pambano la kwanza la raundi ya kwanza ya michuano ya Kombe la Shirikisho.
Kikosi cha timu hiyo kimeeleezwa kipo tayari kwa pambano hilo, japo itawakosa baadhi ya nyota wake ambao wamepatwa na matatizo ya kiafya wakiwa njiani, lakini waliosalia wameapa kupigana kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi hiyo ya leo kabla ya kurudiana na wapinzani wao nchini wiki mbili zijazo.
Azam inahitaji ushindi wa aina yoyote ili kujiwekea mazingira mazuri kwa mechi ijayo mwezi Aprili, hasa ikizingatiwa kiu yao kubwa ni kuona inafika mbali na kuonyesha mfano kwa klabu nyingine za Tanzania ambazo kwa miaka nenda rudi zimekuwa zikiiwakilisha nchi bila ya tija yoyote ya maana.
Afisa Habari wa Azam alinukuliwa jana akisema kuwa kikosi chao kipo imara na wamekuwa wakichimbwa mkwara na mashabiki wa timu yao wakionyeshwa kuwa leo watagongwa mabao mawili au matatu.
"Mashabiki wa mpira wa hapa kila tunapopita wanatuonyesha vidole viwili wengine vitatu kama ishara kwamba tutanyukwa na timu yao mabao hayo, lakini sisi tumekuja hapa kwa ajili ya kupata matokeo mazuri," alisema Jaffar Idd Maganga 'Mbunifu'
Blog hii kwa niaba ya wasomaji wake wote wanaitakia kila la heri Azam iweze kupata ushindi mnono ili iendelee kuipeperuha bendera ya Tanzania kimataifa baada ya wawakilishi wetu wengine, Simba na Jamhuri Pemba kushindwa kuhimili vishindo mapema kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

No comments:

Post a Comment