STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 17, 2013

Twanga Pepeta kuzindua Miss Tabata 2013 Pasaka


BENDI ya muziki wa dansi ya Africans Stars 'Twanga Pepeta' inatarajiwa kuzindua utambulisho wa warembo watakaochuana kwenye shindano la urembo la Tabata 'Miss Tabata 2013' siku ya Pasaka.
Utambulisho huo unatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Da West Park, Tabata jijini Dar es Salaam, ambapoa bendi hiyo maarufu kama 'Kisima cha Burudani' ndiyo itakayotoa burudani.
Mratibu wa shindano hilo Godfrey Kalinga alisema mashabiki na wapenzi wa fani ya urembo watapata fursa ya kuwaona warembo kabla ya fainali itakayofanyika Mei mwaka huu.
Utambulisho wa Miss Tabata 2013 imedhaminiwa na Konyagi, CXC Africa, Fredito Entertainment, Saluti 5 na Kitwe General Traders na kuandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts.
Mratibu huyo alisema warembo 25 wanaendelea na mazoezi kila siku katika ukumbi wa Da’ West Park, Tabata.
Washindi watano kutoka Tabata watafuzu kushiriki Miss Ilala baadaye mwaka huu.
Anayeshikilia taji la Miss Tabata ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.

No comments:

Post a Comment