STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 17, 2013

Mapinduzi Simba! Wanachama wamng'oa Rage

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Mkutano wa Dharura ulioitishwa na wanachama wa klabu ya Simba umeung'oa uongozi wa juu wa klabu hiyo unaoongozwa na Mwenyekiti Ismail Aden Rage aliyepo kwenye matibabu nchini India.
Habari hizo zinasema maamuzi hayo yamefikiwa kwenye mkutano huo uliofanyika na kumalizika mchana huu kwenye ukumbi wa Starlight Mnazi Mmoja, Dar es Salaam na kukabidhi majukumu ya klabu kwa kamati maalum inayoongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Usajili, Zakaria Hanspope na Rahma Al Kharoos.
Hanspope na Bi Rahma maarufu kama Malkia wa Nyuki wataiongoza Simba mpaka pale utakapofanyika uchaguzi mkuu wa kupata viongozi wapya wa klabu hiyo.
Taarifa kamili juu ya mkutano huo tunazifuatilia kwa kuwa MICHARAZO haikuhabatika kuwepo ukumbini hapo na tutawajulisha hivi punde.

No comments:

Post a Comment