STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 25, 2013

Madhira amlilia Rais Kikwete




MUIGIZAJI mahiri wa filamu, Mbwana Salim 'Bessa' au Madhira, amemlilia Rais Jakaya Kikwete na kuomba kuonana naye ili aweze kumfikishia kilio chake na cha wasanii wenye ulemavu kama yeye.
Bessa ambaye pia ni mtunzi wa riwayana mchoraji, alisema kutokana na wasanii wenye ulemavu kutothaminika wala kutiwa moyo, angependa kuonana na Rais Kikwete akiamini anaweza kusikia kilio chao na kuwasaidia ili nao wawe na hadhi sawa na wasanii wengine nchini.
"Ningependa nipate nafasi ya kuonana na Rais Kikwete ili nimfikishie kilio tulichonacho sisi wasanii wenye vipaji vya sanaa, lakini tunadhalilika kwa sababu ya ulemavu wetu, tafadhali naomba unifikishie ujumbe wangu kwa mheshimiwa," alisema Bessa.
Msanii huyo ambaye ni mtunzi mkuu wa vichekesho na filamu za kampuni ya Al Riyamy alisema hali wanayotendwa wasanii wenye ulemavu nchini ikiwemo kunyonywa kimasilahi na kutothaminika hata kwa viongozi wanaosimamia sanaa inawakatisha tamaa, ilihali waliamua kujitegemea.
"Wapo watu wenye ulemavu kama sisi walikata tamaa na kuwa tegemezi, sisi tumeamua kutumia vipaji vyetu kujiajiri na kuwatia moyo wengine, lakini bado tunaangaliwa kama watu duni na kukatishwa tamaa, naimba serikali iliangalie hili," alisema msanii huyo.
Aliongeza kuwa, pamoja na juhudi anazozionyesha akiwa pia ni mwalimu wa chekechea, mchoraji na mtengenezaji wa chaki na batiki, alisema kuna haja wasanii waenye vipaji kama yeye watupiwe macho kuwafanya wapige hatua kimaendeleo na kuwahamasisha wengine kujitegemea.

No comments:

Post a Comment