STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 25, 2013

Golden Bush yazidi kutoa dozi ikiisubiri Wahenga FC

Kikosi cha Golden Bush Veterani
SIKU chache kabla ya kuvaana na wapinzani wao, timu ya Golden Bush Veterani imeendelea kutoa dozi baada ya mwishoni mwa wiki kuinyuka Kibangu Veterani kwa mabao 4-1 kabla ya kuwakung'uta tena watoto zao Golden Bush Fc kwa magoli 2-0.
Mechi hizo za kujipima nguvu zilichezwa Jumamosi na Jumapili ikiwa ni maandalizi ya kuvaana na wapinzani wao, Wahenga Fc pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Tp Afrika, Sinza siku ya Pasaka.
Katika mechi yao dhidi ya Kibangu, Golden Bush walipata ushindi wao kupitia mabao ya Sadik Muhimbo aliyefunga mara mbili, Said Swedi 'Panucci' na Di Natale, huku bao la kufutia machozi la Kibangu liliwekwa kimiani na Daudi.
Katika mechi iliyochezwa jana, dhidi ya vijana wao wanaoshiriki Ligi ya TFF- Kinondoni, Wazee wa Golden walipata ushindi wa 2-0 na kuendeleza ubabe kwa watoto hao kwani wiki iliyopita waliwanyuka mabao 2-1.
Katika hatua nyingine, Mlezi wa Golden Bush Veterani, Onesmo Waziri 'Ticotico' ameamua kutangaza dau kwa wapinzani wao iwapo wataibuka na ushindi au kuambulia sare atakuwa tayari kuwapa papo hapo kitita cha Sh 200,000.
Mechi hiyo ya Golden Bush na Wahenga, inatarajiwa kuhudhuriwa na mgeni rasmi, Kamanda Thobias Andengenye na itachezwa majira ya saa 10 jioni ambnapo lineup ya Golden Bush, kwa mujibu wa msemaji wao itakuwa kama ifuatavyo;

Philemon, Said Swedi, Faraji, Majuto Komu, Wisdom Ndlovu, Godfrey Bonny, Onesmo Wazir 'Ticotico' (captain), Waziri Mahadhi  'Mandieta', Athumani Machupa 'Magoli', Herry Morris na Sadik Muhimbo.

No comments:

Post a Comment