STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 22, 2013

Niyonzima 'atikisa' kiberiti Jangwani


Haruna Niyonzima
KIUNGO wa kimataifa wa Yanga, Haruna Niyonzima, amesema kuwa atakuwa tayari kusaini mkataba mpya wa kuichezea Yanga katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara endapo watampa dola za Marekani 150,000 (Sh. milioni 240).
Mkataba wa Niyonzima aliyejiunga na Yanga mwaka juzi akitokea APR ya Rwanda unamalizika mwezi Juni mwaka huu.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka kwao Kigali, Rwanda ambako amekwenda kuitumikia nchi yake inayokabiliwa na mechi dhidi ya Mali Jumapili, Niyonzima, alisema hataki kurudia makosa aliyofanya mwaka jana.
Niyonzima alisema anaamini kuwa hicho kiwango cha fedha ndiyo dau lake kwa sasa au zaidi na ameamua kuwaambia Yanga kutokana na hatua yao ya kukataa kumruhusu mwaka jana kujiunga na El Mereikh ya Sudan iliyokuwa imekubali kumlipa kiasi hicho.
Kiungo huyo ambaye ni nahodha wa timu ya taifa lake (Amavubi), aliongeza kuwa hivi sasa kazi ya kuzungumzia mkataba wake itafanywa na wakala wake.
"Mambo nahitaji yafanyiwe kazi kabla sijaamua kuendelea kubaki Yanga, ikiwamo kuongezewa mshahara,'' alisema Niyonzima.
Kiungo huyo kipenzi cha mashabiki wa Yanga aliongeza kuwa hataki kupoteza nafasi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma wakati alipokuwa akiichezea APR ambao hawakuwa tayari kumruhusu kirahisi kuondoka ndani ya timu hiyo inayotetea ubingwa wake wa ligi Kuu ya Rwanda.
Akizungumzia matakwa hayo ya Niyonzima, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Seif Ahmed, alisema jana kuwa wako katika mipango ya kuwapa mikataba mipya wachezaji wao wote wanaowahitaji kuendelea kuwa nao kabla ya kumalizika kwa ligi.
Hata hivyo, Ahmed alisema hawawezi kusema ni lini watakamilisha kazi hiyo kwani hiyo ni mipango ya viongozi wa klabu kwa kushirikiana na benchi kao la ufundi.
Niyonzima na Mrisho Ngassa wa Simba waliivutia El Mereikh baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mashindano ya Kombe la Chalenji yaliyofanyika mwaka jana nchini Uganda lakini Ngassa aliamua kuikacha timu hiyo kwa madai kwamba anazingatia maslahi yake na siyo kukimbilia kucheza nje. Nafasi ya nyota hao ilichukuliwa na Selemani Ndikumana kutoka Interclub ya Burundi.


CHANZO:NIPASHE.

No comments:

Post a Comment