STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 26, 2013

Bayern Munich waizima Dortmund na kutwaa Ubingwa Ulaya

Top of the pile: Bayern Munich are the Champions of Europe for a fifth time after beating Borussia Dortmund
Wachezaji wa Bayern wakishangilia na taji lao la Ulaya jana

Dutch delight: Arjen Robben settled the Champions League final with a late, late strike
Aerjen Robben akishangilia bao lake
HUU ni msimu ni Bayern Munich! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mabingwa hao wa Ujerumani kunyakua taji la Ligi ya Ulaya usiku wa kuamkia leo kwa kuwanyuka mahasimu wao Borussia Dortmund kwa mabao 2-1.
Winga wa Kiholanzi, Arjen Robben ndiye aliyewahakikishia wakali hao wa Ujerumani ambao wamekuwa na msimu mzuri mwaka huu kwa kufunga bao dakika za lala salama la pambano hilo.
Robben alifunga bao katika pambano hilo la fainali lililochezwa kwenye uwanja wa Wembley, London nchini England na kuipa Bayern taji hilo lililokuwa halina mtu baada ya waliokuwa mabingwa watetezi, Chelsea kulitema mapema.
Mholanzi huyo alifunga bao hilo tamu dakika ya 89, na pia ndiye aliyetoa pasi ya bao la kwanza la mabingwa hao wapya wa Ulaya lilitumbukizwa kimiani na Mario Mandzukic katika dakika ya 60.
Dortmund iilijipatia bao lake dakika saba baada ya kutanguliwa kufungwa na wapinzani wao kupitia mkwaju wa penati wa Ilkay Gundogan baada ya Mario Reus kuangushwa langoni mwa Bayern na Dante.

No comments:

Post a Comment