STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 15, 2013

Chelsea, Benfica vitani Europa League

Chelsea wakishangilia moja ya mabao yao

BENFICA wamejaaliwa zaidi kiufundi  kuliko Chelsea lakini wataingia katika mechi ya fainali ya Ligi ya Europa leo mjini Amsterdam wakiwa hawapewi nafasi, kwa mujibu wa kocha wa zamani wa England, Sven-Goran Eriksson.
Kocha huyo Msweden anawafahamu vyema Benfica baada ya kuwafundisha mabingwa hao mara mbili wa Ulaya.
"Hakika, Chelsea ndiyo inayopewa nafasi zaidi kutoka na kuwa na kikosi kilichokamilika kila idara lakini kwa mtazamo wangu wachezaji wa Benfica ni 'mafundi' zaidi," Eriksson aliliambia gazeti la kila siku la aBola.
"Kiufundi Benfica wana makali zaidi. Wanamiliki mpira vizuri sana na wachezaji soka zuri."
Mabingwa hao wa Ulaya wa kwaka 1961 na 1962 watawategemea viungo wao 'mafundi' Eduardo Salvio, Nicolas Gaitan, Pablo Aimar, Ola John na Nemanja Matic kumlisha mshambuliaji wao wa Paraguay anayelijua goli, Oscar Cardozo na patna zake wa mashambulizi na Lima na Rodrigo.
Cardozo, Lima na Rodrigo wamefunga magoli 71 katika mechi 118 za klabu hiyo msimu huu.
Eriksson, ambaye aliiongoza timu hiyo ya Ureno wakati ilipolala 1-0 dhidi ya AC Milan katika fainali ya Kombe la Ulaya mwaka 1990 mjini Vienna, anaamini Benfica watasahau haraka kipigo cha 2-1 kutoka kwa mahasimu wao wa jadi Porto Jumamosi.
Chelsea inaweza kuomba dondoo za wapinzani zao kutoka kwa wachezaji wao wa kimataifa wa Brazil, David Luiz na Ramires, ambao wote walisajiliwa kutoka timu hiyo ya Ureno.
Nahodha John Terry huenda akapata pigo jingine kwa mwaka wa pili mfululizo baada ya kukosa pia fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa mwaka jana waliyoshinda kwa 'matuta' dhidi ya Bayern Munich kutokana na kufungiwa. Beki huyo huenda ashindwe kuanza baada ya kutengua 'enka' katika mechi waliyoshinda 2-1 dhidi ya Aston Villa Jumamosi.
Vikosi vinavyotarajiwa:
Benfica: 1-Artur; 34-Andre Almeida, 4-Luisao, 24-Ezequiel Garay, 25-Melgarejo; 22-Nicolas Gaitan, 18-Eduardo Salvio, 21-Nemanja Matic, 35-Enzo Perez; 7-Oscar Cardozo, 11-Lima.
Chelsea: 1-Petr Cech, 28-Cesar Azpilicueta, 4-David Luiz, 2-Branislav Ivanovic, 3-Ashley Cole; 7-Ramires, 8-Frank Lampard, 13-Victor Moses, 10-Juan Mata, 11-Oscar, 9-Fernando Torres.

Refa: Bjorn Kuipers (Uholanzi)

No comments:

Post a Comment