STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 15, 2013

Mradi wa usafiri wa Boti Dar umefikia pazuri




MCHAKATO wa kuanzishwa kwa usafiri wa kutumia Boti kwa wakazi waliopo kando ya Bahari ya Hindi ili kuwapunguzia kero na msongamano kwenye usafiri wa barabarani upo katika hatua nzuri, uongozi wa Jiji la Dar es Salaam umedokeza mapema leo.
Aidha uongozi huo wa jiji hilo umewapongeza wabunge kwa kupitisha bajeti wa Wizara ya Ujenzi ambayo imeipa kipaumbele uboreshaji wa miundo mbinu ya jiji hilo, licha ya kukiri kwa hali halisi fedha zilizotengwa kutatua kero ya msongamano Dar es Salaam ni ndogo, ila wanashukuru kufikiriwa.
Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Abdallah Chaurembo alisema mpango wa jiji kusaidia kero ya msongamano kwa kutaka kuanzisha mradi wa boti zitakazokuwa zikiwahudumia wakati wa maeneo ya Kunduchi na Mbweni kutokea katikati ya jijini (Bandarini) upo katika hatua nzuri.
Meya Chaurembo alisema hivi karibuni uongozi wao ulikutana na wahisani kutokana China ambao waliwaelezea juu ya mipango hiyo na kuahidiwa kusaidiwa na hivyo kuwataka wakazi wa jijini kuondoa hofu kwani wakati wowote mradi huo utaanza kufanyiwa kazi ili kuwatatulia kero ya usafiri.
"Suala la mradi wa usafiri wa bori kutoka bandari kuelekea maeneo ya Kunduchi, Mbweni na Bagamoyo mchakato wake upo katika hatua nzuri sawea na ule wa ujenzi wa barabara nyingine za kupunguza kwero ya msongamano hasa baada ya kukutana na wahisani wetu wa China," alisema.
Chaurembo alitoa ufafanuzi huo katika mahojiano yake na kipindi cha Kumepambazuka cha Radio One kilichosika asubuhi, ambapo alieleza pia furaha yao ya kupitiwa kwa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ambayo safari hii imetengeza fedha nyingine kwa ajili ya kutatua  kero ya usafiri jijini Dar.
Hata hivyo Naibu Meya huyo alisema pamoja na fedha zilizotengwa kwa jiji lao katika bajeti ya mwaka huu kuwa nyingi, bado hazitoshi kulinganisha na hali halisi ya tatizo lililopo Dar es Salaam hasa kartika suala la kuwawezesha kulipa fidia kwa waathiriwa na upitishwaji wa miradi ya ujenzi wa barabara.
Alisema hata hivyo pamoja na kwamba fungu la fedha lililotengwa halijitoshelezi kulinganisha na hali halisi iliyo jijini humo, lakini wanashukuru na kufurahi kuona kilio chao cha muda mrefu kimesikilizwa na wabunge hao.
Juu ya miradi ya ujenzi wa barabara inayoendelea jijini humo ikiwamo ule wa mabasi ya kwenda kasi, alisema wanashukuru inaendelea vyema na kuwaahidi wananchi kwamba itakamilika kulingana na mikataba iliyoingiwa baina ya wakandarasi na serikali hivyo wananchi watulie na kuvumilia kwa sasa.

No comments:

Post a Comment