STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 15, 2013

Maproo Azam FC waanza likizo, kuikosa JKT Oljoro


Kikosi cha Azam Fc
BAADA ya kutwaa nafasi ya pili kwenye ligi kuu msimu wa 2012/2013 kocha wa Azam FC Stewart Hall amewapa likizo wachezaji wake wa kimataifa hivyo hawatacheza mechi ya mwisho ya kumaliza ligi dhidi ya JKT Oljoro itakayochezwa siku ya Jumamosi mkoani Arusha.

Wachezaji hao wamechangia kiasi kikubwa cha kuifikisha timu katika mafanikio hayo pamoja na kufanya vizuri kwenye mechi za kimataifa za Kombe la Shirikisho Afrika ambapo timu hiyo ilimaliza ikiwa imecheza mechi sita katika hatua tatu za mashindano hayo makubwa barani Afrika.

Akizungumza na www.azamfc.co.tz kocha Stewart aliwataja wachezaji hao kuwa ni Kipre Tchetche, Michael Bolou wa Ivory Coast, Humphrey Mieno na Jockins Atudo wa Kenya pamoja na mshambulia Brian Umony wa kutoka nchini Uganda.

Stewart amesema ameamua kuwapa mapumziko wachezaji hao ili wakae pamoja na familia zao kwa muda mrefu kutokana na mechi ya mwisho haitakuwa na umuhimu sana zaidi ya kumalizia ratiba kwa kuwa wameshapata nafasi ya pili na pia wametoa mfungaji bora.

“Kwangu kumpumzisha Kipre ni kutokana na mchezaji huyo kufunga magoli mengi ambayo hayatafikiwa na mchezaji yoyote, pia tumepata ushindi wa pili hivyo nimeona waende nyumbani kwa kuwa ni muda mrefu hawajakaa na familia zao” amesema Stewart.

Azam FC Jumamosi, Mei 18, itamaliza mechi zake za ligi kuu ikiwa ugenini dhidi ya JKT Oljoro kwenye mchezo utakaochezwa uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha, Azam FC inacheza mechi hiyo ikiwa na pointi 51, mshambuliaji Kipre amefikisha jumla ya magoli 17 ya kufunga.

Akizungumzia mchezo huo kocha Stewart amesema kikosi cha mechi hiyo ya mwisho kitaundwa na wachezaji wa ndani ambao watashirikiana pamoja na wachezaji vijana waliopo katika timu yake.

Michael Bolou na Tchetche Kipre wanatarajiwa kuondoka siku ya Alhamisi kuelekea kwao nchini Ivory na wachezaji wa Tanzania wataanza mapumziko yao mara baada ya kumaliza mchezo wa ligi kuu siku ya Jumamosi.

No comments:

Post a Comment