STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 26, 2013

After Death ya kumuenzi Kanumba kutolewa hadharani Jumanne


FILAMU maalum kwa ajili ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo 'After Death' inatarajiwa kuachiwa rasmi mtaani kuanzia kesho.
Filamu hiyo iliyotungwa na Jacklyne Wolper na kuongozwa na Leah Richard 'Lamata' kama njia ya kuenzi kipaji na mchango wa marehemu Kanumba imeshirikisha wasanii kadhaa nyota waliowahi kufanya kazi na mkali huyo aliyefariki mwaka mmoja uliopita.
Akizungumza na MICHARAZO muda mfupi uliopita, Lamata alisema filamu hiyo iliyozinduliwa siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kanumba Aprili 7 mwaka huu itaachiwa kesho Jumanne baada ya taratibu zote kukamilika kwa wasambazaji wao.
Alisema anaamini filamu hiyo itarejesha kumbukumbu za majonzi kwa mashabiki wa marehemu Kanumba, lakini pia watapata burudani baada ya kupita mwaka mmoja tangu wampoteze nyota huyo aliyekuwa akitamba kimataifa.
"Hayawi hayawi sasa yamekuwa, ile filamu ya kumuenzi marehemu Kanumba iliyochezwa na wakali karibu wote waliowahi kufanya kazi na mkali huyo iitwayo 'After Death' itaachiwa rasmi siku ya Jumanne ya Julai 30," alisema Lamata.
Lamata aliwataja baadhi ya wasanii waliocheza filamu hiyo ni pamoja na chipukizi walioibuliwa na Kanumba, Hanifa Daud 'Jenifer' na Othman Njaidi 'Patrick'.
Pia ndani yake wamo wakali kama Ruth Suka 'Mainda', Samsha Ford, Stanley Msungu, Patcho Mwamba, Ben Branco, Wolper, Irene Paul, Uncle D aliyeshabiana na marehemu Kanumba na wengineo.

No comments:

Post a Comment