STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 26, 2013

Simba, Coastal kuvaana Mkwakwani J2


TIMU ya soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam inatarajiwa kuvaana na 'ndugu' zao, Coastal Union ya Tanga katika pambano la kirafiki na kujiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Agosti 24 litakalochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani siku ya Jumapili.
Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema lengo la mechi hiyo ni pamoja na kuwaandaa wachezaji wao kabla ya kuanza kampeni ya kuwania kurejesha taji lao walilolipoteza kwa mahasimu wa jadi, Yanga.
Alisema mechi hiyo itatoa nafasi kwa mashabiki wa Simba waliopo jijini Tanga kuwafahamu wachezaji wapya waliosajiliwa kwa ajili ya msimu mpya.
Alisema mara baada ya mechi hiyo wachezaji wa Simba watarejea jijini Dar es Salaam kujiandaa na mechi nyingine dhidi ya timu ya Kombaini ya Majeshi itakayopigwa Agosti 3 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Coastal itavaana na Simba ikiwa na kumbukumbu ya kuinyuka URA kwa bao 1-0, huku Simba ikiwa inauguza kipigo toka kwa Wakusanya ushuru hao wa Uganda waliowadungua mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment