STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 12, 2013

Bondia Afa ghafla mazoezini, ni 'Tembo Mtoto'

BONDIA Yohana Mathayo 'Tembo Mtoto' amefariki dunia jioni ya jana akiwa mazoezini kwake eneo la Kigogo Mburahati Dar es Salaam.
Kifo hicho kilimkuta ghafla wakati akifanya mazoezi ya kujiandaa na mpambano wake wa ubingwa uliopangwa kufanyika hivi karibuni.
Taarifa za kifo cha bondia huyo aliyekuwa akizidi kupanda chati nchini miongoni mwa mabondia vijana, zilitolewa na kocha wake Kwame Mkuruma, aliyedai mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwao Manzese na huenda akasafilishwa kwenda kuzikiwa kwao mkoa wa Tanga.
Mungu ametoa na Mungu ndiye aliyetwaa. Roho yake ilale mahali pema ila Yohana Mathayo 'Tembo Mtoto' utakumbukwa daima na wadau wenzako wa ngumi umetangulia nasi tu nyuma yako.
Bondia huyo mwenye rekodi ya kucheza michezo 7 ya ngumi za kulipwa akiwa ameshinda mara 4 na kupigwa mara moja na  droo mara mbili.  Marehemu huyo enzi za uhai wake  alijiunga na ngumi za kulipwa mwaka 2011 ambapo mchezo wake wa kwanza kacheza na Seba Temba wa Morogoro ambapo alitoa nae droo na mchezo wake wa mwisho kucheza ni Agosti 9 mwaka huu ambapo alishinda kwa TKO ya raundi ya pili dhidi ya Shujaa Keakea.

No comments:

Post a Comment