STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 17, 2013

Newz Alert: Shule ya Ilboru yafungwa, kisa...!

Waziri Majaliwa alipowahi kwenda kuutuliza mgogoro wa wanafunzi wa Ilboru mwaka jana
TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa, serikali imeamua kuifunga kwa muda usiojulikana Shule Maalum ya vipaji ya Ilboru ya jijini Arusha, baada ya kuwepo kwa tishio la kuchomwa moto kutokana na mgogoro uliodumu kwa muda mrefu shuleni hapo.
Imedokezwa wanafunzi wapatao wanne wanahojiwa kutokana na tishio hilo huku wengine karibu 800 wamerudishwa makwao mpaka watakapotangaziwa vinginevyo.
Tangu mwaka jana shule hiyo imekuwa na mgogoro baina ya wanafunzi na uongozi wake kiasi Naibu waziri wa Tamisemi (Elimu), Kassim Majaliwa kulazimika kuingilia kati, lakini hali haijatengemaa hadi hivi karibuni tena kiliponuka tena.

No comments:

Post a Comment