STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 26, 2013

Kijogoo wa Jakaya agtaka wasanii wenzake kubadilika wathaminike


MUIGIZAJI anayetamba na kundi la kundi la Jakaya Arts, Boniface Gilliard 'Kijogoo', amewataka wasanii wenzake kutambua nafasi zao ndani ya jamii na kuepuka kujihusisha na mambo ya hovyo kwa madai yanachangia hata kuwanyima tenda za matangazo ya biashara.
Kijogoo anayefahamika pia kama 'Kikoti', alisema kujihisha na skendo mara kwa mara mbali na kuonyesha ujinga walionao baadhi ya wasanii, lakini pia inawanyima nafasi ya kulamba 'tenda' za matangazo ya biashara kama wanavyoneemeka wasanii wenzao wa kimataifa.
"Wasanii lazima wabadilike, watambue nafasi zao mbele ya jamii. Skendo zimekuwa zikichafua sifa ya tasnia na wasanii kwa ujumla na hii inatufanya tuendelee kudharauliwa na kupuuzwa kwa sababu ya wachache wasiojitambua na wanaoendekeza ujinga," alisema Kijogoo.
Kijogoo alijipatia umaarufu mkubwa kwa uigizaji wake kupitia michezo kama 'Riziki', 'Barafu la Moyo', 'Mapito', 'Donda la Kichwa', 'Ulimbo' na 'Chekecheo', alisema ni lazima wasanii wajue wao ni kioo cha jamii hivyo wanapaswa kuwa mfano bora katika maneno na matendo yao.
Alisema ni jambo gumu jamii kuwaelewa wasanii katika kile wanachokifikisha kwao kupitia kazi zao iwapo wenyewe wanafanya mambo ya ovyo na yasiyo ya mfano bora ambayo pia huharibu baada ya vijana na watoto wakiwa miongoni mwa mashabiki wao wanaowafuatilia kwa karibu.
Msanii huyo anayeshiriki pia filamu kadhaa kama 'Mahaba Niue', ' Like Father Like Son', 'XXL' na Best Palyer', alisema wasanii wanapaswa kuthamini fani hiyo kwa vile ni ajira yao na tegemeo la kuwainua kiuchumi kama watajikita kwenye kazi kuliko skendo chafu.

No comments:

Post a Comment