STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 26, 2013

Bw' Misosi sasa avuta raha

Joseph Rushahu 'Bwana Misosi
NYOTA wa zamani wa muziki wa kizazi kipya nchini, Joseph Rushahu a.k.a 'Bwana Misosi', ameamua kuvunja ukimya kwa kupakua wimbo mpya uitwao 'Vuta Raha'.
Akizungumza na MICHARAZO, Misosi alisema wimbo huo ameurekodia katika studio za Plexity Records chini ya maprodyuza Zest ba Fide Touch.
Misosi alisema tayari wimbo huo ameuachia mwishoni mwa wiki na tayari umeanza kurushwa hewani kupitia vituo vya redio, mitandao ya kijamii na kupigwa katika kumbi za disko.
Msanii huyo aliyewahi kutamba nchini kwa vibao vikali kama 'Nitoke Vipi', 'Mabinti wa Kitanga' na 'Mungu Yupo Bize', alisema wimbo huo mpya ni kati ya kazi zake mpya alizopanga kuzitoa kabla ya kufungia mwaka 2013.
Misosi ambaye mapema mwaka huu alijitosa kwenye masuala ya filamu, alisema kwa sasa anajipanga ili kutengeneza video ya wimbo huo kabla ya kuachia kazi nyingine za kufungia mwaka na kuukaribisha mwaka mpya.
"Baada ya kimya kirefu nimeachia wimbo mpya uitwao 'Vuta Raha' nilioimba na mwanadada aitwaye Namcy na tayari umeshaanza kuwa gumzo katika vituo vya redio na kumbi za disko, nafurahi ulivyopokelewa," alisema Misosi.

No comments:

Post a Comment