STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 25, 2013

Shule ya Mwandege Boys yatoa msaada wa vitabu vya Sh Mil 3 Mwandege SM


Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mercy Sillah (kushoto) alianza kwa kusalimiana na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwandege., Joseph Awino kabla uya makabidhiano ya vitabu hivyo. Picha ni hatua kwa hatua mpaka vitabu hivyo vyenye thamani ya Sh. Milioni Tatu vilipokabidhiwa.










UONGOZI wa Shule ya Sekondari ya Mwandege Wavulana iliyopo Mkurunga, Pwani imetoa msaada wa vitabu mbalimbali vyenye thamani ya Sh. Milioni Tatu kwa Shule ya Msingi ya Mwandege ili kusaidia na kukuza kiwango cha taaluma kwa wanafunzi wa shule hiyo.
Vitabu hivyo vinavyohusisha kamusi na vile vya masomo mbalimbali kwa Shule ya Msingi vilikabidhiwa juzi kwa shule hiyo katika sherehe za mahafali ya tano  ya kidato cha nne ya Shule ya Mwandede Wavulana yaliyofanyika jana katika shule yao wilayani humo.
Mkuu wa Shule wa Mwandede Wavulana, Enock Walter, alisema uongozi wa Shule yao chini ya Bodi ya Wakurugenzi wametoa vitabu hivyo kwa lengo la kusaidia kuinua kiwango cha elimu kwa wanafunzi wa shule ya Mwandege ambayo ipo jirani nayo.
Mwl Walter, alisema kwa kuwa wao ni wadau wakubwa wa elimu na wanatambua kufanya vyema kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi ni kuzisaidia Shule za Sekondari kupata wanafunzi bora ndiyo maana wamejitolea kutoa zawadi hiyo aliyoamini itasaidia japo ni ndogo.
Mkuu wa wilaya ya Mkuranga, Mercy Sillah, aliyevikabidhi vitabu hivyo kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwandege, Joseph Awino, alisema kilichofanya na uongozi wa Shule ya Mwandege Wavulana ni mfano wa kuigwa na wadau wengine wa elimu nchini.
DC huyo, alisema lau wadau wengine wa elimu wangekuwa wakifanya kama ilivyofanya Shule ya Mwandege Wavulana ni wazi kiwango cha elimu ya Tanzania kingepaa, huku akifichua miongoni mwa shule za msingi wilayani humo zinazofanya vyema ni Mwandege.
Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwandege, Joseph Awino aliishukuru shule ya Mwandege Wavulana kwa msaada huo na kuahidi kuvitumia kwa lengo la kuongeza kiwango cha elimu na ufaulu kwa wanafunzi wake zaidi na ilivyo sasa.
"Tunashukuru kwa msaada huu na Mungu awazidishie Mwandege Boy's na tunaahidi kutumia vitabu hivyo kama vilivyokusudiwa kwa lengo la kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wetu ambao baadhi wanaweza kusoma hapa, ahsanteni sana," alisema Mwl Awino.

No comments:

Post a Comment