STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 1, 2013

Yanga kurejea kileleni kwa mgongo wa JKT Ruvu?

Yanga wataendelea kushangilia leo kama hivi
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga leo ina nafasi kubwa ya kurejea kileleni iwapo itapata ushindi mbele ya JKT Ruvu katika mfululizo wa mechi za raundi ya 12 itakayochezwa uwanja wa Taifa.
Yanga yenye pointi 22 kutokana na kucshuka dimbani mara 11, iwapo itaiangusha JKT ambayo imepoteza yale makali yake iliyopanza nayo ligi ilipoanza miezi mitatu iliyopita, itafikisha jumla ya pointi 25 na kuziengua Azam na Mbeya City waliotangulia kileleni ambao wana piinti 23.
Hata hivyo Yanga, haipaswi kuwadharau JKT Ruvu inayonolewa na kocha mahiri, Mbwana Makatta kwani huenda isikubali kugeuzwa ngazi na mabingwa hao kwenye uwanja wa Taifa.
Kocha Msaidizi wa Yanga, Fred Felix Minziro, alisema kikosi chao kipo imara kwa ajili ya pambano hilo japo kuna baadhi ya majeruhi na kiungo wao nyota, Haruna Niyonzima aliyeenda kwao Rwanda kwa matatizo ya kifamilia watakosekana kwenye pambano hilo la leo.
Wachezaji watakaoungana na Niyonzima kulikosa pambano hilo kutokana na kuwa majeruhi ni beki wa kushoto, David Luhende na kiungo mshambuliaji Nizar Khalfan'.
Minziro alisema pamoja na kuwakosa wachezaji hao, lakini wamejiandaa kuendeleza wimbi la ushindi kwa sababu wachezaji waliosalia bado ni imara na wana ari kubwa ya kuipa ushindi Yanga iliyopo nafasi ya tatu kwa sasa ikitangulia watani zao Simba ambao jana walilazimishwa sare ya 1-1 na Kagera Sugar.
Upande wa JKT Ruvu, kocha wake Mbwana Makatta alinukuliwa na kituo cha redio kwamba wanahisi uchovu wa safari waliokuwa nao ukawagharimu baada ya gari lao kuharibika njiani juzi wakirejea jijini toka mjini Tabora walipoenda kucheza na Rhino Rangers na kunyukwa bao 1-0.
Mbwana alisema hata hivyo watapigana kiume kuhakikisha hawapotezi pambano hilo, japo maafande hao kwa siku za karibuni wamekuwa mdebwedo kwa kufungwa mfululizo baada ya awali kushinda mechi tatu mfululizo.
Vijana hao wa JKT kwa sasa wana pointi 12 tu baada ya kucheza mechi 11, wakishinda nne na kufungwa saba na kuleta hisia kilichoikumba msimu uliopita iliponusurika kushuka daraja huenda ikarejea tena msimu huu japo ni mapema wakati duru la kwanza likiisha wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment