STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 20, 2014

News Alert! Ajali yaua 13 Singida


HABARI zilizotufikia hivi punde kutoka Singida zinasema watu 13 wamefariki dunia baada ya kutokea ajali ya magari mawili kugongana uso kwa uso eneo la Isuna mkoani humo.

Habari hiuzo zinasema ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Toyota Noah na lori ambayo namba zake za usajili hazikupatikana mara moja. Watu 13 waliofariki walikuwa katika Noah iliyokuwa ikitokea Itigi na maiti zao zimehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Singida.

Baada ya ajali hiyo, dereva wa lori na msaidizi wake walitokomea kusikojulikana, ila habari zaidi zinaendelea kufuatiliwa.


No comments:

Post a Comment