STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 20, 2014

Mashetani Wekundu waning'inizwa tena, Spurs yaua

Eto'o akishanglia moja ya mabao yake matatu aliyofunga akiiangamiza Mashetani Wekundu

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/72380000/jpg/_72380954_tottenham-adebayorafp.jpg
Emmanuel Adebayor akifunga moja ya mabao yake mawili jana wakiiua Swansea City ikiwa kwao

WASHAMBULIAJI nyota toka barani Afrika, Emmanuel Adebayor na Samuel Eto'o jana waling'ara baada ya kuziwezesha timu zao za Tottenham Hotspur na Chelsea kuibuka videdea katika Ligi Kuu ya England.
Adebayor alifunga mabao mawili wakati Spurs wakiizamisha Swansea City nyumbani kwa mabao 3-1, naye Eto'o alifunga hat-trick wakati Mashetani Wekundu wakining'izwa 'darajani' na Chelsea.
Eto'o alifunga mabao mawili kipindi cha kwanza katika dakika ya 17 na 45 na jingine dakika ya nne baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, huku bao la kufutia machozi ya Manchester United likifungwa na mtokea benchi Javier Hernandez 'Chicharito' dakika ya 78.
Beki tegemeo wa Man Utd Nemanja Vidic alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 90 na kuifanya Mashetani hao kuzidi kunyong'onyea kabisa.
Katika pambano la Spurs dhidi ya wenyeji Swansea City, Emmanuel Adebayor alifunga mabao yake katika kila kipindi la kwanza kifunga  dakika ya 35 kabla ya kuongeza jingine lililokuwa la tatu katika pambano hilo kwenye dakika ya 71.

Bao jingine lililoisaidia Spurs kupata ushindi huo mnono lilifungwa na Chico aliyejifunga dakika 53, na bao la kufutia machozi la Swansea lilifungwa na Wilfried Bony dakika ya 78.

No comments:

Post a Comment