STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 27, 2014

Newz Alert! Watu 11 wapoteza maisha katika ajali mjini Tanga


Taswira kutoka eneo la Mkanyageni baada ya ajali hiyo mbaya iliyoua watu 11.

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa watu 11 wamefariki dunia huku wengine wakijeruhiwa katika ajali mbaya eneo la Mkanyageni mkoani Tanga.
Inadaiwa kuwa ajali hiyo ilisababishwa na gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 410 BJD kugongana na Scania namba T 605 ABJ asubuhi hii.
Katika ajali hiyo, Coaster lilikuwa likitoka mkoani Tanga kwenda Lushoto na madereva wa magari yote mawili hawajulikani walipo baada ya ajali.
Miili ya marehemu katika ajali hiyo imehifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza, Tanga.

Taarifa zaidi zitawajia baadaye ila MICHARAZO inatoa pole kwa wote walioguswa na ajali hiyo na kuwaombea waliitangulia mbele ya Haki Roho zao ziweke mahali Pema na majeruhi wapone haraka.

No comments:

Post a Comment