STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 27, 2014

Real Madrid, Bayern waongoza tuzo za Kikosi Bora Ulaya

http://english.ahram.org.eg/Media/News/2014/4/24/2014-635339446265357238-535.jpgKLABU ya Real Madrid ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wamethibitisha ubora na thamani yao baada ya kutoa wachezaji nane katika uwaniaji wa tuzo ya kikosi bora cha Ulaya.
Tuzo hiyo ya Uefa ya mwaka 2014 itakayotolewa hivi karibuni inajumuisha pia wachezaji wanne kutoka AtleticoMadrid ambao pia wanaiwania.
Wanaowania kuingia kwenye 1st Eleven ya mwaka ya Uefa ni kama ifuatavyo;
Kutoka Madrid : Carvajal, Ramos, Kroos, Modric, James, Bale, Benzema na Cristiano Ronaldo.
Bayern wenyewe wametoa wachezaji sawa kama Real Madrid nao ni Neuer, Alaba, Benatia, Boateng, Lahm, Xabi Alonso, Müller na Lewandowski.
Upande wa Atletico Madrid iliyotoa wachezaji wanne ambao ni Koke, Arda, Godín na Miranda.
Wengine waliopo kwenye kinyang'anyiro hicho ni Xabi Alonso (Bayern Munich) na Di María (Manchester United), Courtois (Chelsea), Diego Costa (Chelsea).
Kwa upande wa Barcelona imetoa wachezaji watatu ambao ni Rakitic, Neymar na Messi. Pia mchezaji wa Red Bull Salzburg Jonathan Soriano naye yupo kwenye mbio hizo za kuwepo kwenye First Eleven.

No comments:

Post a Comment