STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 24, 2014

Maskini! Sheikh Ponda kuendelea kusota rumande


KATIBU wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Nchini, Shekhe Ponda Issa Ponda, ataendelea kukaa rumande hadi Januari 5, mwaka 2015 pale kesi yake itakapotajwa tena, baada ya jana Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mkoa wa Morogoro kushindwa kuanza kusikilizwa na kutoa dhamana yake. 
Hatua hiyo ilitokana na kufuatia mawakili wa pande mbili za mashtaka ya utetezi, kuvutana kuhusiana na mshtakiwa kupewa dhamana na kuondolewa mashitaka. Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, Mary Moyo, ambapo mawakili wa pande mbili hizo walizua mabishano ya vifungu vya sheria kuhusu kuanza rasmi kusikilizwa kwa kesi hiyo pamoja na mtuhumiwa kupewa dhamana ama laa. Ponda alifunguliwa kesi namba 128/2013 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, akikabiliwa na mashtaka matatu ambayo aliyatenda Agosti 10, mwaka 2013 katika eneo la Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro na alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Augosti 19 mwaka 2013. 
Hata hivyo, Ponda alifikishwa mahakamani hapo majira ya saa 3.15 asubuhi akiwa ndani ya gari ndogo lenye namba za kiraia T 278 CSM huku akisindikizwa na magari ya Polisi, ambapo waumini wachache waliruhusiwa kuingia chumba cha Mahakama , ambamo alikuwemo pia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro , Leonard Paul , kusikiliza kesi hiyo. Waumini waliobaki nje ya uzio, walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za kumtukuza Mola na wengine waliendesha swala pembezoni mwa uzio wa mahakama hiyo hadi pale kesi hiyo ilipoahirishwa. Polisi waliwaamuru kutawanyika kwa njia ya amani eneo hilo na walitii agizo hilo.

No comments:

Post a Comment