STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 18, 2015

Hapatoshi leo England, Man City vs Arsenal

KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea leo kwa mechi mbili likiwamo linalovuta hisia za wengi litakalochezwa kwenye uwanja wa Etihad mjini Manchester kati ya wenyeji Manchester City dhidi ya Arsenal.
Pambano jingine la leo litazikutanisha timu za West Ham Utd watakaokuwa nyumbani kuwakaribisha Hull City katika uwanja wa Boleyn.
Mabingwa watetezi Manchester City wataikaribisha Arsenal wakitoka kulazimishwa sare katika mechi yao ya mwisho, ilihali Arsenal wakitoka kupata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Stoke City.
Ingawa Arsenal itakosa huduma za beki wake Mathieu Debuchy aliyeumia bega katika mechi yao iliyopita sambamba na kuwakosa wakali wengine ambao ni majeruhi kama ambavyo watetezi Man City watakavyokosa huduma za wakali wake akiwamo Yaya Toure na Wlifried Bony waliopo Afrika kwa sasa..
City itakuwa ikisaka ushindi nyumbani kuweza kuendelea kuwabana Chelsea wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo wakati wao wakiwa wapo nafasi ya pili.
Watetezi hao wana pointi 47 wakati wapinzani wao Arsenal wakiwa na pointi 36 wakishika nafasi ya tano.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa pambano moja tu litakalozikutanisha timu za Everton dhidi ya West Bromwich Albion mechi itakayochezwa kwenye uwanja wa Goodson Park.

No comments:

Post a Comment