STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 19, 2015

Ally Mustafa 'Barthez' ni Nouma sana!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2gWCT-X80QbEFaBLH3ow-j-DUBUoiESu7HybsUaOTaiK29nZu8xGcFRQwETVHpw-nbY11UkU2DDjhKczuGFnfxgBd_5QO8ZU6Kvpo1vd4IHZkFNaX3sIoyhhtPOFOXUbpjMPWPETf4lkv/s1600/35.jpg
Barthez mbele kushoto akiwaongoza wachezaji wenzakle wa Yanga
PAMBANO la Yanga dhidi ya Prisons-Mbeya lililochezwa uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya kwa vijana wa Jangwani wakiibuka na ushindi wa mabao 3-0 umezidi kumpandisha chati kipa Ally Mustafa 'Barthez' ambaye amedaka mechi sita mfululizo za Ligi Kuu Tanzania Bara bila kuruhusu bao lolote.
Kipa huyo aliyekuwa na wakati mgumu mbele ya kikosi cha Jangwani tangu Yanga ilipolazimishwa sare ya mabao 3-3 na Simba Oktoba mwaka juzi, hajafungwa bao lolote katika muda wa dakika 540 huku kwenye uwanja wa Sokoine akigeuka kuwa shujaa kwa kuokoa michomo mingi ya wachezaji wa Prisons.
Hizo ni mbali na dakika 90 za pambano la kimataifa la Kombe la Shirikisho Afrika ambapo Yanga ilishinda mabao 2-0 na yeye akiwa kwenye milingoni mitatu ya lango ya vijana wa Jangwani.
Barthez aliyesajiliwa na Yanga akitokea Simba, rekodi zake zinaonyesha kuwa ameshuka dimba katika mechi hizo kama ifuatavyo na kuwafunika makipa wote wa timu nyingine 13 zinazoshiriki ligi hiyo.
Jan 17, 2015Yanga vs Ruvu Shooting (0-0)
Jan 24, 2015Polisi Moro vs Yanga (1-0)
Feb 01, 2015Yanga vs Ndanda (0-0)
Feb 4, 2018Coastal Union vs Yanga (0-1)
Feb 08, 2015Yanga vs Mtibwa Sugar (2-0)
 Feb 14, 2015-Kimataifa
Yanga vs BDF XI (2-0)
Feb 19, 2015
Prisons vs Yanga (0-3)

No comments:

Post a Comment