STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 19, 2015

BAHANUZI, MAHUNDI WANG'ARA VPL

http://2.bp.blogspot.com/-ORUnNfNV-xE/VM0wOPMp6vI/AAAAAAABdBc/1sAbma_8dB4/s1600/BAHANUZI.jpg
Said Bahanuzi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2NUIe7-6s8hh3LAnWZphC1Sfmct-j1gnFK6vBlYl6-vWAkEms7KvbsXk8lsXx7as54qc9WOVhCaehk3-wlIYA3DXm_G5D2mryGl3IxaJ0IKhGMNNPLYmPUTtm0N9aOnG0wHywciFMsGQ/s1600/IMG_1197.jpg
Mahundi (kulia) akichuana na Niyonzima katika moja ya mechi ya Ligi Kuu
KIUNGO wa timu ya Coastal Union ya Tanga, John Mahundi amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba 2014 wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mahundi alitoa mchango mkubwa kwa timu yake ya Coastal Union mwezi huo na kuchaguliwa na jopo la makocha linalofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora wa kila mwezi.
Aidha mshambuliaji wa timu ya Polisi Morogoro, Said Bahanuzi 'Spider Man' amechaguliwa kuwa mchezaji bora mwezi Januari 2015.
Bahanuzi anayechezea timu ya Polisi Moro kwa mkopo akitokea timu ya Young Africans amekua na mchango mkubwa kwa timu yake tangu kujiunga nayo mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom nchini.
Kwa kuibuka wachezaji bora, Mahundi na Bahanuzi watazawadiwa fedha taslimu Sh. Mil. 1/ kwa kila mmoja kutoka kwa wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.
Jopo maalum la makocha waliopo katika viwanja vyote vinavyotumika kwa mechi za Ligi Kuu ndiyo wanaofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora kwa kila mechi kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.
Baadaye alama zao kujumlishwa ili kumpata mshindi wa mwezi.

No comments:

Post a Comment