STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 19, 2015

Yanga wafanya mauaji Mbeya, Azam yabanwa

Yanga
Msuva na Coutinho walipokuwa wakijiandaa kuiangamiza Prisons-Mbeya

Azam
Azam walishindwa kushangilia kama hivi leo kwa Ruvu Shooting
KLABU ya Yanga imeendeleza rekodi yake ya kugawa dozi kwa wapinzani wao katika Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kuilaza Prisons-Mbeya kwa mabao 3-0 na kukwea kileleni mwa msimamo wakiiengua Azam.
Azam waliokuwa uwanja wa Mabatini-Mlandizi wameshindwa kutamba kwa kulazimishwa suluhu mbele ya maafande wa Ruvu Shooting na kutoa nafasi kwa Yanga kuwaacha kwa pointi mbili kileleni.
Kwa suluhu iliyopata kwa Ruvu, imeifanya mabingwa watetezi Azam kufikisha pointi 26 na kushuka hadi nafasi ya pili licha ya timu zote mbili kulingana mechi zote zikicheza michezo 14 kila moja.
Yanga ikicheza kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya walipata ushindi huo murua na uliowafanya kufikisha pointi 28 baada ya kupata mabao yake mawili katika kipindi cha kwanza na jingine kipindi cha pili.
Mabao hayo yaliwekwa kimiani na Simon Msuva aliyefunga dakika ya tatu tu ya mchezo kabla ya Coutinho kuongeza la pili.
Msuva alirudi tena kambani kwa kufunga bao la tatu kipindi cha pili na kumfanya afikishe jumla ya mabao sita akibakisha mabao mawili kumkuta Didier Kavumbagu wa Azam mwenye mabao nane.
Yanga wataendelea kusalia jijini humo kwa ajili yua kusubiri pambano lake la Jumapili dhidi ya Mbeya City kabla ya kutimka zao Botswana kuwafuata BDF XI kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika mchezo wao wa kwanza uliochezwa mwishoni mwa wiki, Yanga iliitambia BDF kwa kuilaza mabao mawili yote yakiwekwa kimiani na Mrundi, Amissi Tambwe.

No comments:

Post a Comment