STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 4, 2015

Prisons yamfurusha Mwamaja, Makatta amrithi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjaJrEavPqz6tdbaPJoZmvtYQffdUBf8ZB4pv78v6DDUEKBlffZJyhLOcc-KGwJFL0hn5CO0P6O5Fj_T_zQU8jrYulHMFe7oQSEzt6e49kVAVtP6uu4macHTa9l2xDasmWECDTPulRIcOs/s1600/mwamaja.JPG
Kocha David Mwamaja aliyesitishiwa mkataba wake na Prisons-Mbeya
KLABU ya Prisons Mbeya imemtimua aliyekuwa Kocha wao mkuu, David Mwamaja na nafasi yake imechukuliwa na Mbwana Makatta aliyewahi kuinoa timu hiyo siku za nyuma.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Prisons, Hassain Yusuph alithibitisha kusitishiwa mkataba kwa kocha Mwamaja na kunyakuliwa kwa Makatta aliyekuwa akiinoa timu ya Ligi Daraja la Kwanza, Oljoro JKT.
Timu hiyo ndiyo inayoburuza mkia katika msimamo wa ligi hiyo wakikusanya pointi 14 tu baada ya jioni ya leo kulazimisha sare ya 0-0 na JKT Ruvu kwenye mchezo uliochez a kwenye uwanja wa Chamazi.
Hassain alisema kuwa mabadiliko hayo yamefanywa kutokana na kocha Mwamaja kushindwa kuiweka pazuri timu hiyo na kocha mpya atainoa timu hiyo kwa kipindi chote kilichofuata cha kumalizia ligi.

No comments:

Post a Comment