STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 4, 2015

Pep Guardiola hana mpango wa kuhama Bayern

http://www.predapublishing.com/the-sportist/wp-content/uploads/2014/10/pg-68-garside-pa.jpgKOCHA wa klabu ya Bayern Munich, Pep Guardiola amesema hana mpango wowote wa kuikacha timu hiyo mwishoni mwa msimu kufuatia kuzuka tetesi kuwa anataka kuhamia Manchester City.
Mkataba wa Guardiola na mabingwa hao wa Bundesliga unatarajiwa kumalizika majira ya kiangazi mwaka 2016 lakini mazungumzo ya mkataba mpya yamesimamishwa hatua iliyozua minong’ono ya kuondoka.
Hata hivyo, Guardiola ameweka wazi kuwa bado anataka kuendelea kuinoa Bayern na hajafanya mazungumzo na klabu nyingine yeyote.
Akihojiwa Guardiola amesema hajapokea ofa yeyote kutoka kwa City kwa klabu nyingine kwani matumaini yake ni kubakia Bayern kwa kipindi kirefu.
Guardiola aliendelea kudai kuwa kwa sasa bado ana mkataba na Bayern na anapenda kuheshimu hilo mpaka hapo watakapokaa tena na kuzungumza juu ya mkataba mpya.

No comments:

Post a Comment