STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 4, 2015

Mtibwa Sugar yazinduka, Ndanda yaiua Ruvu

Mtibwa Sugar waliozinduka
Polisi Moro waliokubali kichapo mbele ya Mtibwa leo
TIMU ya Mtibwa Sugar wametakata kwenye uwanja wa nyumbani baada ya kuicharaza Polisi Moro kwa mabao 2-1 katika pambano lililochezwa uwanja wa Manungu Complex
Mtibwa ambao kwa muda mrefu walikuwa hawajashinda walipata mabao yake kupitia kwa Ally Shomari na Said Mkopi baada ya awali wageni wao kuitangulia kufunga bao kwa mkwaju wa penati kupitia Said Bahanuzi.
Kwa ushindi huo Mtibwa wamepanda hadi katika nafasi ya tano wakifikisha pointi 22.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Ndanda Fc ya Mtwara iliitambia nyumbani Ruvu Shooting kwa kuilaza mabao 2-1 katika pambano kali lililochezwa uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani.
Ndanda walianza kuandika bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza kabla ya kuongeza jingine kupitia kwa Omega Seme na wenyeji Ruvu walijipatia bao la kufutia machozi dakika za lala salama.
Bao hilo lilifungwa na Yahya Tumbo na kuifanya Ndanda kufikisha pointi 19 wakati Ruvu wakiswaliwa na pointi 21.
Ligi hiyo itaendelea tena siku ya Jumamosi na Jumapili kutakapochezwa pambano la watani wa jadi Simba na Yanga.

No comments:

Post a Comment