STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 12, 2016

Hakuna ujanja FDL yafikia mwisho nani kupanda Daraja?

Lyon na Ashanti katika mechi yao
PATAMU! Ligi Daraja la Kwanza Bara (FDL), imefikia patamu kwani wikiendi hii, lazima kieleweke wakati mechi za kufungia msimu zitakapopigwa.
Licha ya kufungia msimu, lakini mechi hizo zitakazochezwa katika muda mmoja bila kujali tofauti mazingira ya hali ya hewa, pia zitatoa timu mbili za mwisho za kupanda daraja kucheza Ligi Kuu Bara msimu ujao wa 2016-2017.
Kwa mujibu wa agizo la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mechi zote zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni, huku makundi ya A na C yakimulikwa kwani ndio yanayoshikilia hatma ya timu mbili za mwisho za kuungana na Ruvu Shooting kucheza Ligi Kuu ijayo.
Kundi C keshoJumamosi itashuhudia michezo minne, ila miwili ndiyo mikali ikizihusisha JKT Kanembwa dhidi ya Geita Gold mjini Kigoma na ule wa Polisi Tabora itakayoialika Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora.
Geita na Polisi zote zina nafasi sawa ya kupanda daraja zikiwa na pointi 27 kileleni, huku zikitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa, japo pia viwanja vingine zitapigwamechi za Mbao dhidi ya Polisi Mara na Panone itakayomalizana na Rhino Rangers .
Katika kundi A African Lyon, Friends Rangers na Ashanti Utd zote zina nafasi ya kufuzu VPL na zote zitashuka uwanjani keshokutwa Jumapili.
Friends itaivaa Kiluvya United pale Chamazi, jijini Dar, Ashanti na Lyon zitamalizana Karume, Dar es Salaam, huku Polisi Dar na Polisi Dodoma zitacheza Uwanja wa Mabatini, Mlandizi na CDA itamalizana na KMC.
Lyon ina pointi 26 ikihitaji sare kurudi Ligi Kuu, wakati Friends na Ashanti kila moja ina pointi 23 zikihitaji kushinda na kuiombea Lyon iteleze ili mojawapo ipande daraja.
Mechi za kukamilishia ratiba ya kundi B zipo hivi; Kimondo itacheza na Kurugenzi, Njombe Mji dhidi ya Lipuli, Ruvu itaikaribisha Polisi Moro na Burkina Faso itavaana na JKT Mlale mjini Morogoro.
Timu mbili za kushuka daraja kuungana na Kanembwa zinatarajiwa kufahamika katika mechi hizo za kesho na keshokutwa.

Msimamo Kundi A
                                   P   W  D  L    F   A  Pts
Africans Lyon                13  8   2  2   17  9  26
Friends Rangers            13  6   5  2   21  10  23
Ashanti Utd                   13  6   5  2   18  11  23
KMC FC                         13  6   4  3   12  10 22
Kiluvya United               13  5   5  3   12   8   20 
Polisi Dar                       13  3   5  5    9  13  14
Polisi Dom                     13  2   1  10  10 23  7
CDA                              13  1   3   9   6   21  6

Msimamo Kundi B
                               P  W  D  L  F  A  Pts
Ruvu Shooting          13  10  2  1  26 7  32
Njombe Mji               13   7   1   5  14  12 22
JKT Mlale                  13   5   6  2  17 10 21
Kurugenzi                 13   6   3  4  16 13 21
Polisi Moro                13  5   2  6   12 17  17
Lipuli Fc                    13   3  5   5   12  15 14
Kimondo                   13   2   3  8   8  22 9
Burkina Faso             13   1   4   8  10 18 7

Msimamo Kundi C
                              P W  D  L  F   A  Pts
Polisi Tabora            13  8  3  2  20  5   27
Geita Gold               13  8  3  2  20  6   27
Oljoro JKT               13  6  4  3  12  14  22
Mbao FC                  13  5  4  4  14  18  19
Panone                    13   4  4  5  16 13  16
Polisi Mara               13   2  7  4  11  15  13
Rhino Rangers          13   2  6  5  8   13  12
JKT Kanembwa         13  0  3  10  7  24  3

Ratiba kamili ya wikiendi hii:
Kesho Jumamosi:
Kimondo FC      vs     Kurugenzi FC    
Njombe Mji       vs     Lipuli FC                      
Ruvu Shooting   vs     Polisi Morogoro    
Burkinafaso FC  vs     JKT Mlale    
Mbao FC            vs     Polisi Mara    
Polisi Tabora       vs     JKT Oljoro    
JKT Kanembwa   vs     Geita Gold FC    
Rhino Rangers    vs     Panone FC    

Jumapili:
Polisi Dar            vs     Polisi Dodoma    
Mji Mkuu             vs     KMC FC                      
African Lyon        vs     Ashanti United    
Friends Rangers   vs     Kiluvya United   
 

No comments:

Post a Comment