STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 12, 2016

Hatimaye Yanga wapaa usiku huu kwenda Mauritius

Picha haihusiani na habari hii. Wachezaji wa Yanga wakiwa katika moja ya safari zao
KIKOSI cha Yanga kilichokwama kuondoka alfajiri ya leo kwenda Mauritius hatimaye kimepaa muda huu kuelekea nchini humo kwa ajili ya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Cercle de Joachim utakaochezwa kesho jioni.
Yanga ilikwama kuondoka na ndege ya ATCL kutokana na kuharibika kwa kifaa kilicholazimika kwenda kununuliwa Afrika Kusini na kufungwa, huku marubani wa ndege hiyo wakitishwa na hali ya hewa ya huko waendako.
Mpaka saa 12 jioni kulikuwa bado kuna hatihati ya safari hiyo baada ya rubani wa ndege kutaka kupimwa kwa watu wote wa msafara ili kuona kama uzito wao utaendana na safari yao wakiwa angani.
Hata hivyo mwishowe saa 1 msafara huo ulipaa kuelekea huko, licha ya kwamba Yanga kuonekana ilishavunja Kanuni ya 8 ya michuano ya CAf juu ya timu wageni kutakiwa kuwa nchi wanayoenda kucheza ndani ya saa 48. Kitu kizuri ni kwamba Mkuu wa msafara wa Yanga, Ayoub Nyenzi aliwasiliana mapema na CAF na wenyeji wao pamoja na kamisaa kuwajulisha juu ya tatizo lao.
Kwa taarifa hiyo, kikao cha mchezo huo (pre-match meeting) ambacho hufanywa siku moja kabla ya mchezo husika kimesogezwa mbele hadi kesho asubuhi na jioni mchezo utapigwa kama kawa, licha ya kwamba Yanga itaingia Mauritius usiku wa manane.
Mwendo wa kutoka jijini Dar es Salaam mpaka Curepipe mji utakaochezwa mchezo huo kwenye Uwanja wa George V ni kama saa nane, hivyo ni wazi Yanga huenda ikafika kati ya saa 9 alfajiri na jioni watashuka dimbani bila hata ya kupasha.
Kosa hilo la kuchelewa kwa Yanga ambayo awali ilikuwa ipae tangu Jumatano kabla ya kubadilishwa kwa ratiba yao, inaweza kuwa faida kwa wenyeji ambao kwa msimu wa pili sasa ndio mabingwa wa taifa hilo la kisiwani katika Bahati ya Hindi.

No comments:

Post a Comment