STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 23, 2010

Al Madina yafuturisha wanawake Dar, wakizundua ofisi



TAASISI ya Huduma za Kijamii ya Al Madinah, 'Al Madinah Social Services Trust' jana jioni ilizindua ofisi yao mpya kwenye jengo la BinSlum Plaza sambamba na kuwafuturisha futari wanawake wa Kiislam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ally Hassani Mwinyi, Mama Sitti Mwinyi aliyeambana na Bi Khadija Mwinyi.
Shughuli hizo za uzinduzi na ufuturishwaji futari, iliandaliwa na Kamati ya Wanawake wa taasisi hiyo ya Al Madinah na kudhaminiwa na benki ya Stanbic na ilifanyika kwenye jengo hilo la Bin Slum lililopo mitaa ya Livingstone na Mkunguni, Kariakoo jijini Dar.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Wanawake wa Al Madinah, Hajat Mariam Dedesi, alisema hafla hiyo ya kuwafuturisha wanawake wa Kiislam ilikuwa na lengo kubwa la kujenga umoja na mshikamano pamoja na kutekeleza moja ya sunna iliyokokotezwa kwenye mfungo wa Mwezi wa Ramadhani ya watu kulishana kwa lengo la kupata dhawabu.
Mariam alisema mbali na hilo, lakini kubwa ni kutaka kutoa hamasa kwa wanawake wa Kiislam kuungana pamoja na kujitokeza kwa wajili ya kwenda Hijja kupitia taasisi yao ambayo inajishughulisha na huduma za kuwasafirisha mahujaji.
Alisema wanashukuru msaada mkubwa waliopewa na benki ya Stanbic, ambayo aliwahimiza wanawake nchini kote kujiunga nayo kwa lengo la kuweza kuhifadhia fedha zao bila ya riba na pia kupata mikopo itakayowawezesha kujianzishia na kuendesha miradi yao ya kimaendeleo kujikuza kiuchumi.
Naye mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Sheikh Ally Mbaraka, alitoa wito kwa waumini wote wanaotaka kwenda hija kujitokeza kujiandikisha na kulipia ada zao kupitia taasisi hiyo akidai ina huduma murua na gharama nafuu wakati wa kwenda na watakapokuwa hija.
Sheikh Mbaraka alisema huduma za malazi, usafiri kupitia Shirika la Ndege la Oman ni zenye kiwango cha hali juu na zitakazowawezesha mahujaji kutosafiri kwenda mbali na miji watakayofanyia hija zao.
Naye meneja wa Stanbic Bank, Bi Jennifer Hillal, alisema ni vema mahujaji na waumini wengine kuchangamkia kujiunga na benki yao kwa kuwa inazingatia miiko na sharia za kiislam kwa kutotoza riba ya aina yoyote.


Ukiondoa mgeni rasmi, Mama Sitti aliyeambatana na 'mkemwenza' Bi Khadija Mwinyi, wengine waliohudhuria ni Mwenyekiti wa

No comments:

Post a Comment