STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 18, 2013

Hali ya hewa Arusha yarejea kwenye utulivu

MOTO UNAWAKA BAADA YA KUCHOMWA MATAIRI


HALI ya utulivu imeanza kurejea jijini Arusha baada ya hali kuchafuka kwa Jeshi la Polisi kufyatua mabomu ya machozi dhidi ya wafuasi na viongozi wa CHADEMA baada ya kukusanyika kwenye viwanja vya Soweto ili kujua namna watakavyoshiriki mazishi ya watu waliouwawa kwa Bomu siku ya Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa toka Arusha zinasema kuwa hali imerejea kuwa tulivu baada ya mshikemshike wa Polisi kuwatimua wananchi hao na kuleta kizaazaa cha kutunishiana misuli na kurejea hali ya taharuki jijini humo baada ya hivi karibuni kukumbwa na matukio yaliyosababisha vifo vya watu wasio na hatia.

No comments:

Post a Comment