STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 18, 2013

Msajili wa vyama alaani mlipuko wa bomu Arusha, avinyooshea kidole vyama vya CCM na CHADEMA

Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania, John Tendwa
Na Suleiman Msuya
MSAJILI  wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa amesema ili kuhakikisha kuwa amani inaendelea kudumu ni muhimu kuwepo kwa uvumilivu na kuheshimiana  kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Kauli hiyo ameitoa leo Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku chache baada ya kutokea kwa mlifuko wa bomu kwenye mkutano wa kampeni ya udiwani uliokuwa unaendeshwa na CHADEMA katika viwanja vya Soweto mjini Arusha.
Tendwa alisema kwa muda sasa kumekuwepo kwa msuguano mkubwa baina ya vyama hivyo viwili jambo ambalo linaonyesha dalili za kuhatarisha amani ya nchi na wananchi kwa ujumla.
Msajili huyo alisema vyama hivyo vinaonyesha kukosa  uvumilivu na kuheshimiana kwani kwa kipindi hiki kifupi cha kampeni za udiwani viomekuwa na fujo ambazo kila mmoja anamshutumu mwenzake jambo ambalo sio nzuri katika nchi.
Alisema kutokana na tukio hilo viongozi wao wameibuka na kushutumiana ambapo  Katibu Uenezi wa CCM Nape Mnauye alisikika akiwashutumu CHADEMA kuhusikana wakati Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akisema CCM na Jeshi la Polisi wanahusika.
“Inasikitisha sana kuona watu wanakufa alafu watu wanajitokeza na kuanza kushutumiana kuwa huyu ndiye anahusika mimi nomba wapeleke ushahidi Jeshi la Polisi ili kuweza kusaidia upelelezi,” alisema.
Tendwa alisema katika kuhakikisha kuwa vyama hivyo vinaendelea kuheshimiana na kuvumiliana anatarajia kuita kikao ambacho kitashirkisha ofisi yake, jeshi la polisi na vyama hivyo kwani wanapoelekea ni pabaya.
Alisema iwapo uchaguzi wa Udiwani hali inakuwa hivyo je itakuwakuaje katika uchaguzi wa Serikali za Mitaaa na uchaguzi mkuu watu watarajie nini kwani ni ishara mbaya kwa Taifa ambalo linasifika kwa amani.
Aidha Msajili huyo alipotakiwa kuelezea juu ya ofisi yake kuvifuta vyama hivyo viwili vya CCM na CHADEMA alisema ofisi yake ina mamlaka hayo ila hiyo ni hatua ya mwisho kuchukuliwa iwapo itabidi.
Tendwa alisema uamuzi wa kuvifuta vyama hivyo unaweza kuwa na athari kubwa kwani utahitaji gharama kubwa za kufanyika uchaguzi jambo ambalo sio la kukimbilia.
Alisema ofisi yake inahitaji kukutana na vyama hivyo  kwani ndio njia sahihi ya kufikia muafaka kwa maslahi ya vyama hivyo na wananchi kwa ujumla.
“Ni lazima jamii itakatumbua kuwa maamuzi haya yanahusi CCM ambayo ipo madarakani ambapo matokeo yake ni kuvunja Serikali na kwa CHADEMA ni kuwaondoa wabunge wake hivyo uchaguzi kufanyika tena,”  alisema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini Peter Mziray amevitaka vyama hivyo kutambua kuwa nchi hii iwapo itaingia vitani wao ndio wahusika wakubwa.
Alisema Baraza hilo linatajia kukutana kwa pamoja likishirikisha vyama vyote vya siasa ambapo watatoka na azimio juu ya hali ilivyo hivi sasa kwani inaonyesha dalili za kupotea kwa amani.
Mziray ambaye ni Rais Mtendaji wa Chama cha African Progressive Party Tanzania (APPT Maendeleo alisema hali inayotoke kwa sasa jeshi la Polisi na vyombo vyote vya usalama vinapaswa kushutumiwa kwani vionyesha kutofanya kazi vizuri.
Mwenyekiti huyo alisema hali hiyo inasikitisha sana kutokana na ukweli kuwa watu wasio na hatia kupoteza maisha jambo ambalo halikubaliki.
“Kwa kweli vyama hivi viwili vimekuwa na matukio mbalimbali ambayo kwa muono wangu nadhani vinahitajika kubadilika kwani hali sio shwari ila vyombo vya usalama pia vina mapungufu yao,” alisema

No comments:

Post a Comment