STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 3, 2010

'Vigogo', Mawaziri wa JK 'chali' CCM







MAWAZIRI kadhaa wa Serikali ya Awamu ya Nne na wabunge wengi waliomaliza muda wao, wameshindwa kuongoza katika mchakato wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM), zilizopigwa juzi kuteua wagombea wa ubunge, ingawa wanachosubiri ni kwa sasa ni hatma yao katika vikao vya juu vya chama hicho.

Baadhi ya mawaziri walioanguka katika kinyang'anyiro hicho ni aliyekuwa Mbunge wa Nkenge,Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diosdorus Kamala pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera wa Korogwe Mjini, huku kukiwa na taarifa kwamba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo, naye ameshindwa kuongoza katika Jimbo la Mbulu.

Mbali na hao, wabunge wengine maarufu wameanguka akiwemo aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, John Malecela wa Mtera, ambaye ameshindwa kushika nafasi ya kwanza ambayo ingempa nafasi ya moja kwa moja ya uteuzi, ingawa wakati mwingine matokeo hayo hubadilishwa na vikao vya juu vya CCM.
Kwa mujibu wa Katibu wa CCM Mkoa huo, John Barongo,Malecela alimbwagwa na Katibu wa CCM wilaya ya Tarime, Livingstone Lusinde ambaye ameongoza kwa kupata kura 5,810 huku Malecela akiwa na kura 5,379.

Jimbo la Mpwapwa, George Lubeleje ambaye ameliogoza jimbo hilo kwa miaka 20, ameangushwa na Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Gregory Teu,Lubeleje aliyeambulia kura 4,830 huku Teu akiongoza kwa kura 7,777.

Jimbo la Chilonwa, matokeo ya awali yanaonesha Hezekiah Chibulunje anaongoza kwa kura 5,267 ambapo Joel Mwaka akiwa na kura 3,848, katika kata 8 kati ya kata 13.

Barongo alifafanua kuwa, kwa upande wa Jimbo la Kondoa Kaskazini, matokeo ya awali yalionesha kuwa Zabein Mhita alikuwa akiongoza ra 6,211, Mohamed Rashid akiambulia kura 2,116.

Jimbo la Kondoa Kusini, matokeo ya awali ya kata 11 kati ya kata 20, mtangazaji wa zamani wa TBC, Juma Nkamia alikuwa akiongoza kwa kura 4,249 huku akifuatiwa na Paschal Degera kura 632 huku aliyekuwa Katibu wa Bunge, Damian Foka akiambulia kura 545.

Jimbo la Kibakwe, George Simbachawene alikuwa akiongoza kwa kupata kura 8,824 akifuatiwa na Acray Galawika mwenye 2,537.Jimbo la Bahi, Donald Mejiti aliongoza kwa kupata kura 2,627 akifuatiwa na Omar Baduel mwenye kura 2,268.

Jimbo la Dodoma Mjini ambalo lilikuwa na wagombea 19, Peter Chiwanga alikuwa akiongoza kwa 3,183 katika kata 18 kati ya kata 37, huku akifuatiwa na David Malole mwenye kura 2,479 naaliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa akipata kura 2,141.

Kwa upande wa Dar es Salaam, matokeo mengi yalikuwa hayajafika katika ofisi za wilaya. Matokeo ya awali katika Jimbo la Temeke yanaonesha kuwa Abass Mtemvu alikuwa anaongoza katika kata nne za Miburani, Sandali na Mtoni.

Alifuatiwakwa mbali na Salimu Chicago wakati Hiza Tambwe katika kata hizo aliambulia nafasi ya tatu. Katika Jimbo la Kigamboni, Faustine Ndungulile alikuwa anaongoza katika kata za Vijiweni, Kimbiji na Mbagala Kuu.

Katika jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu anaongoza na kuwaacha wapinzani wake kwa mbali huku katika Jimbo la Ukonga, Godwin Barongo anaongoza katika kata za Gongo la Mboto, Ukonga, Pugu na Kitunda.

Kwa upande wa Jimbo la Kinondoni aliyekuwa anaongoza ni Idd Azzan ambaye matokeo ya awali katika kata za Kijitonyama, Kigogo, Hananasif pamoja na Mwananyamala huku Shy-Rose Bhanji akimfuatia kwa karibu. Kura za majimbo ya Segerea, Kawe na Ubungo yanatarajiwa kutolewa leo.

Mkoani Kilimanjaro, Mbunge aliyemaliza muda wake katika Jimbo la Vunjo, Aloyce Kimaro, ameanguka baada ya kushika nafasi ya pili kwa kubwagwa na Wakili Crispin Meela.

Akitangaza matokeo hayo, Katibu wa CCM mkoani Kilimanjaro, Stephen Kazidi alisema katika Jimbo la Vunjo, Kimaro alipata kura 3,194, Meela kura 7,162 huku wagombea wengine akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Taifa, James Kombe akipata kura 1,110 na Thomson Moshi kura 788.

Jimbo la Moshi Mjini aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kiusa katika Manispaa ya Moshi, Buni Ramole alishinda kwa kura 1,554 huku wagombea wengine na kura zao katika mabano wakiwa Thomas Ngawaiya (1,539), Justine Salakana (1,152), Gibson Lyamuya (269) na Joseph Mtui (208). Wengine ni Onesmo Ngowi (127), Peter Njambi (110), Athumani Mwariko (109) na Askofu Pius Ikongo (91).

Jimbo la Moshi Vijijini, Dk. Cyril Chami aliongoza kwa kupata kura 9,196 huku mpinzani wake wa karibu, Ansy Mmasi akipata kura 2,791.

Jimbo la Mwanga, Mbunge anayemaliza muda wake, Profesa Maghembe alipata kura 10,743, Joseph Thadayo kura 6,889 na Karia Magalo alipata kura 252.

Hata hivyo, Katibu huyo wa CCM Mkoa, amesema Ngawaiya ameandika barua akilalamika kwamba baadhi ya wanachama wamezuiwa kupiga kura jambo lililomnyima kura ambazo zingempa ushindi.

Jimbo la Rombo, Kazidi alisema Basil Mramba ameongoza kwa kura 8,389, Netburga Masikini kura 2,946, Lemunge Lesfory kura 854 na Stambul Vitus kura 779.

Jimbo la Same Magharibi, Dk. Mathayo David ameongoza kwa kura 14,281, sawa na asilimia 95, akifuatiwa na John Singo kura 608, Ali Kibwede kura 65 na Lameck Shogholo kura 61.

Jimbo la Hai, Mbunge anayemaliza Fuya Kimbita aliongoza kwa kura 3,725, akifuatiwa na Dastan Mallya (2,649), Aziz Waziri (2,384), Christopher Awinia (1,149), Masumba Meena (939), Lazaro Swai (728), Neema Massawe (456) na Gasper Ngido.

Katika Jimbo la Siha, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri alipita bila kupingwa ndani ya CCM.

Jimbo la Same Mashariki, Mbunge aliyemaliza muda wake, Anne Kilango Malecela, ameongoza kwa kupata kura 7,514 akifuatiwa na mpinzani wake mkubwa, Michael Kadede aliyepata kura 1,804.

Mkoani Singida, Singida Mjini, Mbunge aliyemaliza muda wake, Mohammed Dewji aliongoza kwa kishindo kwa kupata kura 8,997, sawa na asilimia 95, Hawa Ngulume kura 390 na Mariam Msawira 35.

Jimbo la Iramba Mashariki, Mgana Msindai ameshindwa baada ya kupata kura 3,005 huku aliyeongoza ni Salome Mwambu aliyepata kura 3,635, jimbo hilo lilikuwa na wagombea tisa.

Jimbo la Iramba Magharibi, aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Juma Kilimbah, amebwagwa pia baada ya kupata kura 3,788 ukilinganisha na aliyeongoza, Lameck Mwigulu mwenye kura 3,834.

Jimbo la Kwimba, Mbunge anayemaliza muda wake, Bujiku Sakila amekiri kushindwa na akizungumza kwa simu na gazeti hili jana kutoka Ngudu, makao makuu ya Wilaya ya Kwimba, alisema atakuwa tayari kumuunga mkono mgombea wa CCM, Shanif Mansoor ambaye ni Mhasibu wa CCM mkoa wa Mwanza.

“Kwanza nimeshindwa vibaya, lakini niseme kutoka rohoni mwangu kabisa ni mfumo wa uchaguzi wa kura za maoni ndiyo ulionifanya nishindwe, lakini sitakuwa na malalamiko makubwa maana nikiyatoa kitahitajika, “evidence,“ na mimi sikushindwa kwa kukosa sifa za kuwa Mbunge ila ni system ya uchaguzi ilivyokuwa, kulikuwa na rushwa sana hapa Kwimba
lakini mkamataji hakuwepo,” alisema.

Naibu Waziri huyo wa zamani aisema kwa jinsi alivyoona mazingira ya uchaguzi wilayani Kwimba, alisema Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) hawakufanya kazi yao barabara ya kudhibiti rushwa katika uchaguzi huo wa kura za maoni kwa madai kuwa rushwa katika jimbo hilo ilikuwa kubwa, kiasi cha kuifafanisha Takukuru na mtoto mdogo na wagombea watu wazima.

Jimbo la Ilemela, Mbunge wake, Anthony Diallo ameongoza kwa kupata kura 6,601. Wagombea wengine na kura zao ni Pastory Masota (2,159); John Buyamba (1,837); Samson Maganga (519); Darius Ngocho (450); DC mstaafu Jared Gachocha (365); Ashery Gasabire (357) na Shadrack Fereshi (343).

Katika Jimbo la Sengerema, kwa mujibu wa Katibu wa CCM, Maiko Kahuruda alisema jana kuwa mbunge ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alikuwa anaongoza kwa wingi wa kura akifuatiwa kwa karibu na Francisco Shejamabu.

Kwa Jimbo la Buchosa, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Dk. Charles Tizeba alikuwa anaongoza akifuatiwa na Eric Shigongo na Mbunge aliyekuwa anashikilia jimbo hilo, Samuel Chitalilo alikuwa wa tatu.

Jimbo la Misungwi, Kahuruda alisema Charles Kitwanga “Mawe Matatu” alikuwa akiongoza kwa kupata kura 9,104 katika kata tisa kati ya 27 zilipokewa matokeo yake huku akifuatiwa na Mbunge aliyemaliza muda wake, Jacob Shibiliti na Madoshi Makene akishika nafasi ya tatu.

Majimbo ya Sumve na Magu, matokeo yao yalikuwa yakiendelea kukusanywa, wakati katika Jimbo la Nyamagana, matokeo ya awali yaliyotolewa jana na Katibu wa CCM Wilaya, Musa Matoroka yalionesha kuwa Mbunge wa sasa, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha alikuwa anaongoza kwa kupata kura 8,627, akifuatiwa na John Marogori aliyepata kura 2420.

Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni Joseph Kahungwa (1,941); David Mtetemera (570); Wilson Swalala (492); Robert Masunya (396); Stephen Deya (286); Maseke Magaiwa (315); Stephen Deya (286); Abdi Chakechake(271); William Mvanga (220); Boniface Kahangara (162); na Ibrahim Lukumay (124).

Jimbo la Ukerewe, Mbunge aliyemaliza muda wake, Balozi Gertrude Mongella ameongoza kwa kura 6,666 na akifuatiwa na Josephat Lyato aliyepata kura 4,140. Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni Msafiri Nyandiga (3,530); Oswald Mwizarubi (2,362); Mtani Chitanda (1,822); Deus Tungaraza (967); Ernest Kamando (642); Majige Munyu (284) na Mwibure

Kazi (104).

Jimbo la Busega, aliyekuwa anaongoza ni Dk. Titus Kamani ambaye alikuwa amemuacha mbali sana Dk. Raphael Chegeni

ambaye ni Mbunge anayemaliza muda wake.

Katika Jimbo la Busanda, Mbunge wa sasa, Lolensia Bukwimba alikuwa akiongoza. Jimbo la Nyang’hwale, Mbunge

anayemaliza muda wake, James Musalika ameshika nafasi ya tatu kwa kura 1,200 wakati DC wa Kilombero, Evarist Ndikilo

ana kura 3,125 na aliyeongoza ni Hussein Gulamali kwa kura 4,449.

Mkoani Shinyanga, Jimbo la Shinyanga Mjini, aliyeongoza kwa mujibu wa Katibu wa CCM Mkoa, Mohammed Mbonde, ni

Stephen Masele akiwaangusha wagombea wengine akiwamo aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na

Mbunge mtetezi, Dk. Charles Mlingwa na Mbunge mwingine wa Viti Maalumu, Joyce Masunga;

Jimbo la Solwa aliyeongoza ni Ahmed Salum; Jimbo la Meatu ni Salum Khamis ‘Mbuzi’; Jimbo la Kishapu ni Suleiman Nchambi’s na Jimbo la Bariadi Magharibi ni Andrew Chenge.

Katibu huyo wa CCM Mkoa aliwataja wengine waliongoza ni Emmanuel Luhahula (Bukombe); Peter Bunyungoli (MaswMashariki); Simon Robert (Maswa Magharibi); Martin Makondo (Bariadi Mashariki); Luhaga Mpina (Kisesa); James Lembeli (Kahama). Katika Jimbo Mbogwe, Augustine Masele anaongoza kwa kura nyingi.

Jimbo la Nkenge, Mbunge aliyemaliza muda wake, Dk. Diodorus Kamala ameanguka kwa kushika nafasi ya pili baada ya nafasi ya kwanza kuchukuliwa na Asumpta Mshamu.

Kamala ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, amepata kura 6,184 wakati Mshama amepata kura

9,055. Wagombea wengine ni Dickson Balyagati (4,123), Julius Rugemarila (771), Charles Katarama (410), Ismail

Suleiman (239) na Amani Kajuna kura 146.

Jimbo la Ngara, Mbunge wa sasa, Profesa Feetham Banyikwa alikuwa anashika nafasi ya tatu kwa kuwa na kura 2,112,

wakati anayeongoza ni Deo Ntukamazima akiwa na kura 3,954 akifuatiwa na Alex Gashaga mwenye kura 3,838.

Jimbo la Chato, Mbunge wa sasa ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. John Magufuli alikuwa akiongoza kwa kura 8,305 akifuatiwa na Dk. Lukanima mwenye kura 810.

Jimbo la Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki amepita bila kupingwa.

Jimbo la Kyerwa, Mbunge aliyemaliza muda wake, Eustace Katagira ameongoza kwa kura nyingi. Hata hivyo, takwimu hazikuweza kupatikana haraka kutokana na tawi mojawapo katika Kata ya Businde kuendelea kukamilisha taratibu za uchaguzi kabla ya kuunganisha matokeo yote.

Jimbo la Karagwe ambalo pia mchakato wa kuunganisha takwimu uliendelea hadi jioni, matokeo yanaonesha mbunge aliyemaliza muda wake, Gosbert Blandes ameshinda kwa kura nyingi. Aliyeshika nafasi ya pili ni Karim na ya tatu ni Profesa Ngalinda.

Jimbo la Bukoba Vijijini ambako hadi jana jioni matokeo ya kata 20 kati ya 29 yalishapatikana, Jasson Rweikiza

ameongoza kwa kura 18,212. Mbunge aliyemaliza muda wake, Nazir Karamagi ameshika nafasi ya pili kwa kura 4,111 na

kufuatiwa na Novatus Nkwama mwenye kura 4,111.

Wagombea wengine ni Muzamir Kachwamba aliyepata kura 816 na Kamalu Mustafa amepata kura 600.

Mbunge wa sasa wa Biharamulo Magharibi, Oscar Mukasa ameongoza kwa kura nyingi akifuatiwa na Agricola Magoho na

Hamidu Nzomukunda.

Kwa upande wa Muleba Kusini, ingawa hadi jioni mchakato wa kuunganisha kura za kata zilizochelewa ulikuwa

ukiendelea, Profesa Anna Tibaijuka ndiye alitajwa kuibuka mshindi kwa kura nyingi akiwaacha mbali Mbunge wa sasa,

Wilson Masilingi aliyeshika nafasi ya pili. Nafasi ya tatu imeshikwa na Alfred Tibaigana.

Maswa Magharibi, Amani Nzugile Jidulalamabambasi, amefariki dunia jana wakati akiwa njiani kutoka Hospitali ya

Wilaya ya Maswa kwenda Rufaa Bugando kwa uchunguzi na matibabu zaidi baada ya kuwa amelazwa katika hispitali hiyo ya

wilaya tangu Julai 29, mwkaa huu.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dk. Amos Mremi alisema mwanasiasa huyo alikuwa amelazwa kwenye hospitali hiyo

kutokana na uvimbe mkubwa uliojitokeza katika sehemu zake za siri na kutokana na hali yake ilivyokuwa ilibidi apewe

rufaa ya kweda Bugando kwa uchunguzi na matibabu, na jana akiwa njiani kwenda Mwanza pamoja na muuguzi mmoja kwenye

gari la wagonjwa, alifikishwa hadi katika mapokezi ya Bugando, lakini mara tu kufika hospitalini, iligundulika kuwa

amefariki dunia.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Bugando, Dk. Charles Majinge alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na kwamba alifikishwa

mapokezi akiwa tayari amefariki dunia, mwili wake ulitarajiwa kurejeshwa wilayani Maswa kwa ajili ya mazishi.

Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa kiongozi wa UDP, alishika nafasi ya tatu nyuma ya Robert na Shibuda, miongoni mwa

wagombea tisa waliojitokeza.

Jimbo la Chalinze, aliyeongoza ni Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Said Bwanamdogo aliyepata kura 8,144 akifuatiwa na

aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Imani Madega mwenye kura 4,193; Mbunge aliyemaliza muda wake, Ramadhan

Maneno kura 3,623. Jimbo hilo lilikuwa na wagombea 10.

Jimbo la Bagamoyo, Mbunge wa sasa Dk. Shukuru Kawambwa ambaye pia ni Waziri wa Miundombinu, ameongoza kwa kura

6,576, akiafuatiwa Dk. Andrew Kasambala mwenye kura 1,061.

Wabunge waliomaliza muda wao, Dk. Ibrahimu Msabaha (Kibaha Vijijini), Dk. Zainabu Gama (Kibaha Mjini); Profesa

Idrisa Mtulya (Rufiji), nao wameanguka.

Wabunge wa zamani waliopeta katika kinyang'anyiro hicho ni Adam Malima (Mkuranga); Abdul Malombwa (Kibiti) na

Abdulkarim Shah (Mafia)

Wagombea wapya waliochomoza na Silvesta Koka (Kibaha Mjini); Hamidu Abuu (Kibaha Vijijini); Seleman Jafo (Kisarawe)

na Dk.Seif (Rufiji).

Hata hivyo, baada ya matokeo hayo kutangazwa, aliyekuwa Mbunge wa Kibaha Mjini, Dk. Gama aliwasilisha barua kwa

Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani, Sauda Mpambalyoto akipinga matokeo ya jimbo lake kwa madai ya uchaguzi kutawaliwa na

mchezo mchafu na rafu za hapa na pale kwa baadhi ya wagombea.

Jimbo la Kasulu Mjini, Neka Raphael ameongoza kwa kura 672 akifuatiwa na Gidion Bunyaga (510); Askofu Gerald Mpango (306); Twalib Mangu (270) na Agnes Nyowola (225).

Jimbo la Kasulu Vijijini, Daniel Nsanzugwanko alikuwa akiongoza kwa kura 1,560 akifuatiwa na Kafonogo Mayengo (625) na Patrick Nyembele (420).

Jimbo la Manyovu, Albert Obama alikuwa akiongoza kwa kura 770; James Japhet (667); Eliadory Kavejuu (300); Betwel Ruhega (300) na mbunge anayemaliza muda wake, Kilontsi Mporogomyi (260).

Jimbo la Muhambwe, Jamal Tamim alikuwa akiongoza kwa kura 2,921 akifuatiwa na Richard Kigaraba (); Mbunge wa sasa, Felix Kijiko (1,523); mbunge wa zamani Arcardo Ntagazwa (577) na Edgar Mkosomali (922).

Mkoani Iringa, hatima ya wabunge Joseph Mungai, Monica Mbega, Jackson Makweta, Profesa Raphael Mwalyosi, Benito

Malangalila na Yono Kevela, kurudi kwa mara nyingine tena katika vikao vya Bunge lijalo, kutategemea zaidi maamuzi ya juu ya vikao vya CCM, baada ya taarifa za awali kuonesha kuwa wameshindwa kura za maoni.

Hata hivyo, mpaka tunakwenda mitambani ofisi za chama za majimbo hayo zilikuwa hazijatoa taarifa rasmi, na Katibu wa CCM wa Mkoa, Mary Tesha alipoulizwa, alisema ofisi yake inaendelea kupokea matokeo kutoka katika majimbo yote ya uchaguzi.

Taarifa za awali za uhakika kutoka katika majimbo hayo zinaonesha kwamba wakati Mahamudu Mgimwa ameibuka kidedea katika Jimbo la Mufindi Kaskazini lililokuwa likiongozwa na Mungai, Deo Sanga (Jah People) ameibuka kidedea katika Jimbo la Njombe Kaskazini lililokuwa likiongozwa na Makweta.

Mbega (Iringa Mjini) ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro atalazimika kurudi haraka iwezakanavyo mkoani humo

kuendelea na majukumu mengine ya kiserikali baada ya kushindwa katika kura hizo zilizompa ushindi aliyekuwa Katibu

Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Frederick Mwakalebela.

Mwakalebela anaongoza kwa kuwa na kura 3,897, Mbega 2,989 na Yahaya Msigwa 1,217. Ludewa, Mbunge wa sasa Profesa

Mwalyosi amebanwa na Deo Filikunjombe ambaye matokeo ya awali yanaonesha amepata kura zaidi ya 6,000 huku Profesa

Mwalyosi akipata kura zaidi ya 4,000.

Dalali maarufu Kevela wa Njombe Magharibi, naye anadaiwa yuko katika wakati mgumu dhidi ya Mbunge aliyemtangulia

Thomas Nyimbo, huku taarifa kutoka Jimbo la Mufindi Kusini nazo zimethibitisha kwamba Benito Malangalila naye

ameshindwa kuongoza katika kura za maoni za jimbo hilo. Mendradi Kigola anaongoza katika jimbo hilo.

Katika Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto ameshindwa kumpiku Mbunge aliyemaliza muda wake, Profesa Peter Msolla

aliyepata zaidi ya kura 18,000 dhidi ya kura zake zinazodaiwa kuwa zaidi ya 3,000.

Jimboni Makete, mbunge aliyemaliza muda wake, Dk. Benelith Mahenge amejihakikishia kurudi bungeni kwa awamu ya pili,

kama ilivyo kwa Njombe Kusini kwa Naibu Spika, Anne Makinda.

Kutoka Isimani, Katibu wa CCM wa wilaya ya Iringa, Luciano Mbosa alisema jana kwamba William Lukuvi ameshinda kura hizo kwa kujinyakulia kura 7,996 dhidi ya kura 533 za Festo Kiswaga, 286 za Leonard Mwali na Yahaya Mtete aliyepata kura 176.

Huko Kalenga, Mbosa alisema shughuli ya ujumlishaji kura inaendelea hata hivyo taarifa za awali zinaonesha kwamba Dk William Mgimwa amepata kura 2,819 akifuatiwa na Abbas Kandoro aliyepata kura 2,353 na Hafsa Mtasiwa aliyepata kura

1,553.

Mkoani Mbeya, Mbarali, Mbunge anayemaliza muda wake, Estherina Kilasi amekuwa wa tatu akiwa na kura 614, huku

akiongoza Modestus Kilufi kura 1,521 na wa pili ni Burton Kihaka (1,322). Ileje ni Aliko Kibona (5,844), Ambonesigwe

Mbwaga (2,200) na Godfrey Msongwa (2,004).

Lupa, Mbunge aliyemaliza muda wake, Victor Mwambalaswa ameongoza kura 6,135 dhidi ya aliyewahi kuwa Mbunge na

Waziri, Njelu Kasaka (4,135). Songwe, Mbunge aliyemaliza muda wake, Dk. Guido Sigonda amepata kura 780; aliyeongoza

ni Philipo Mulugo (7,100); Paul Ntwina (1,618) na Hamad Juma (962).

Kyela, Mbunge ambaye alikuwa kinara katika mapambano ya ufisadi, Dk. Harrison Mwakyembe ameongoza kwa kura 7,681 dhidi ya George Mwakalinga (574) na Elias Mwanjala (512).

Rungwe Mashariki, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya ameongoza kwa kupata kura 4,240 dhidi ya Stephen Mwakajumulo (228). Rungwe Magharibi, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa ameongoza kwa kura 6,974, dhidi ya Richard Kasesela (5,843) na Frank Magoba (1,379).

Mbeya Mjini, Mbunge aliyemaliza muda wake, Benson Mpesya ameongoza dhidi ya Mbunge wa Kuteuliwa, Thomas Mwang’onda kwa kupata kura 5,586 dhidi ya kura 3,362.

Mbeya Vijijini, Mbunge aliyemaliza muda wake, Mchungaji Luckson Mwanjale ameongoza kwa kura 7,353 dhidi ya kura 1,902 za Andrew Saile.

Mkoani Tabora, Jimbo la Urambo Mashariki, Samuel Sitta alikuwa akiongoza kwa kura 6,130 dhidi ya Masoud Maswanya

mwenye kura 2,432 na Ali Karavina kura 464. Jimbo la Urambo Magharibi (sasa Kaliua), Profesa Juma Kapuya anaongoza

kwa kura 5.656 dhidi ya Ramadhan Kalla mwenye kura 751.

Jimbo la Nzega, Hussein Bashe alikuwa akiongoza kwa kura 6,815 na Lucas Selelii ambaye niMbunge aliyemaliza muda

wake, ana kura 1,420.

Jimbo la Bukene, Mbunge aliyemaliza muda wake, Teddy Kasella-Bantu ana kura 1,968 na Suleiman Zeddy ana kura 1,727.

Sikonge ni George Kakunda anaongoza kwa kura 1,570 dhidi ya Mbunge anayemaliza muda wake, Said Nkumba mwenye kura

1,365.

Tabora Mjini, Ismail Aden Rage anaongoza kwa kura 4,145 dhidi ya Mwanne Mchemba ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu

mwenye kura 2,985 na mbunge wa jimbo hilo, Siraju Kaboyonga ana kura 835.

Mkoani Lindi, Jimbo la Mchinga, Said Mtanda alikuwa akiongoza katika kata nane kati ya 10, kwa kuwa na kura 3,768

dhidi ya kura 1,577 za Mbunge aliyepita, Mudhihir Mudhihir.

Jimbo la Nachingwea, Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe ameongoza kwa kura 5,887, akifuatiwa na DC wa

zamani wa Bukoba Mjini, Albert Mnali (3,912), Elias Masala (1,844), Maokola Majogo (1,191), Ally Mpelemba (450),

Fulgence Mpelembe (126) na Benito Ng’itu (266).

Mkoani Katavi, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amepita bila kupingwa katika Jimbo la Mlele (zamani Mpanda Mashariki),

lakini wabunge watatu wa zamani wameanguka.

Jimbo la Sumbawanga Mjini, Aeshy Hillaly ameongoza kwa kupata kura 867 dhidi ya Mbunge wa Viti Maalumu, Elieta

Switi 155; Edson Makallo (54); James Kusulo (26); Frolence Mtepa (25); Emmanuel Msingezi (18); Joseph Malikawa

(38).

Jimbo la Nkasi Kaskazini, ameongoza Mohamed Keissy (1,557); Hiporitus Matete (1,173), DED wa Kilosa, Ephrem

Kalumalwendo (1,003), mbunge anayemaliza muda wake, Ponsiano Nyami (695), S. Khamsin (319) na V. Konga (51). Jimbo

la Nkasi Kusini, aliyeongoza ni Desderius Mipata (719); Joseph Walingozi (348); Emmanuel Sungura (45); J. Mwanansau

(23); Joseph Kitakwa (58).

Jimbo la Kwela, ameongoza Ignas Malocha (5,772); Meja January Kisango (1,772); Didas Mfupe (1,669); Steven

Chambanenje (796); Patrick Maufi (329); Solomon Jairos (66) na Bendicto Chapewa (227). Jimbo la Kalambo, Josephat

Kandege ameongoza kwa kura (5,597) dhidi ya Ludovick Mwananzila (4,061) na Paul Mwanandeje.

Mkoani Mtwara, Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia ameongoza katika Jimbo la

Mtwara Vijijini huku Vita Kawawa akiongoza Jimbo la Namtumbo.Mkoani Tanga, Bendera ameshindwa na Yussuf Nasir kwa

kupata kura 2,258 dhidi ya Nasir aliyeongoza kwa kura 2,513.

Pangani, Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, ameshinda Mbunge aliyemaliza muda wake, Risherd Abdallah kwa kura 4,391 dhidi ya 2,442.

Tanga Mjini, Omar Nundu ameongoza kwa kura 7,445 dhidi ya Harith Mwapachu aliyepata kura 2,156 ambaye ni Mbunge aliyemaliza muda wake.

Wakati huo huo, aliyekuwa Mbunge wa Tarime kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Charles Mwera ameshindwa kutetea kiti hicho baada ya kubwagwa na mwanachama mwenzake, Mwita Waitara ambapo Waitara alipata kura

131 akifuatiwa na Mwera aliyepata kura 113. Wagombea John Heche kura 92 na Philipo Nyanchini aliyepata kura 10.

Upande wa Viti Maalumu kwa wagombea wa Chadema Tarime aliyeshinda ni Mary Nyagabona aliyepata kura 58 na kuwashinda Ester Matiko aliyepata kura 54, wengine ni Tekra Johanes kura nne na Mwenyekiti wa Wanawake wa Chadema Taifa, Leticia Mosore hakupata kura.

No comments:

Post a Comment