STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 19, 2012

Mashujaa, Mashauzi kung'arisha Miss Tabata

BENDI zinazotamba nchini kwa sasa Mashujaa na Mashauzi Classic zitatumbuiza kwenye kinyang'anyiro cha kumtafuta mrembo wa Tabata kitakachofanyika Juni Mosi katika ukumbi wa Da West Park, Tabata. Mratibu wa shindano hilo, Godfrey Kalinga alisema wameamua kuweka burudani yenye ladha tofauti ili kukidhi kiu ya watu mbalimbali watakaohudhuria shindano hilo. Kalinga alisema siku hiyo pia itatumika kusherehekea miaka 10 tangu kuasisiwa kwa shindano la Miss Tabata. "Shindano la mwaka huu litakuwa ni la aina yake kwa sababu utakuwa ni mwaka wetu wa 10 tangua kuanza kuandaa Miss Tabata... ndio maana tunaleta burudani nyingi," alisema mratibu huyo wa Bob Entertainment na Keen Arts. Alisema warembo waliyowahi kushinda mataji mbalimbali ya shindano hilo, pia wamealikwa kusherehekea miaka 10 ya Miss Tabata. Shindano hili limedhaminiwa na Dodoma Wine, Redds, Integrated Communications, Fredito Entertainment, Multichoice Tanzania, Screen Masters, Kitwe General Traders, Step In Electronics, Brake Point, Atriums Hotel na Lady Pepeta. Warembo 10 wa kwanza watafuzu kushiriki Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania. Mrembo anayeshikilia taji la Tabata kwa sasa ni Faiza Ally. Warembo wa Tabata wamekuwa wakifanya vizuri katika mashindano ya Miss Tanzania ambapo 2010 Consolata Lukosi alishinda nafasi ya tatu kabla ya kutangazwa kuwa balozi wa kinywaji cha Redds.
Visura watakaochuana kinyang'anyiro cha Miss Tabata 2012

No comments:

Post a Comment