STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 19, 2012

Doyi Moke awataka Yanga watulie

KIPA nyota wa zamani wa klabu za Majimaji-Songea, Simba na Yanga, Doyi Moke, amewasihi wanachama wa timu ya Yanga kumaliza matatizo yao kwa kukaa mezani na kuzungumza. Aidha, kipa huyo raia wa JK Congo na aliyewahi kuzidakia pia timu za Rayon Sport ya Rwanda na Vital'O ya Burundi, alisema wanayanga wanapaswa kukumbuka kuwa mbele yao kuna kibarua cha kutetea taji la Kombe la Kagame la klabu bingwa za Afrika Mashariki na Kati hivyo watulizane mapema. Akizungumza kwenye mahojiano maalum, mkali huyo ambaye kwa sasa ni mfanya biashara madini alisema Yanga watajuta mbeleni wasipokaa mezani. "Nadhani hali inayoendelea Yanga haileti ishara njema, pande zinazotofautiana zikae chini na kuzungumza, kuendelea kulumbana bila kupata muafaka ni kuiweka pabaya timu yao wakati wanakabiliwa na michuano ya Kombe la Kagame linaloanza Juni," alisema. Alisema hadhani kama kuendelea kujadili kipigo cha mabao 5-0 walichopewa na watani zao Simba au kupokonywa taji la ligi kuu itaisaidia klabu hiyo wakati matokeo hayo hayawezi kubadilika. Baadhi ya wanachama wa Yanga wamekuwa wakishinikiza mwenyekiti Lloyd Nchunga ajiuzulu mara moja, na katika kuhakikisha hilo wameitisha mkutano mkuu kesho klabuni huku mwenyekiti akiwa ametaja Julai 15 kuwa siku ya mkutano mkuu rasmi wa mwaka.
Doye Moke enzi akicheza soka nchini Tanzania

No comments:

Post a Comment