STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 19, 2012

'Ticotico' wa Simba aanzisha klabu binafsi ya soka, kuteta leo

ALIYEWAHI kuwa Katibu wa Kamati ya Fedha ya klabu ya Simba, Onesmo Waziri 'Ticotico' ameanzisha klabu ya soka iitwayo 'Golden Bush Fc', ambayo imeshasajiliwa rasmi tayari kwa ajili ya ushiriki wa michuano mbalimbali. Akizungumza na MICHARAZO, Ticotico, mmoja wa 'membaz' wa zamani wa Friends of Simba, alisema klabu yake imesajiliwa ndani ya wilaya ya Kinondoni na itakuwa na makao makuu yake eneo la Mabibo, Dar es Salaam. Alisema mpaka sasa timu hiyo imeanza kukusanya wachezaji chini ya kocha wa muda, nyota wa zamani wa timu ya Yanga, Waziri Mahadh 'Mandieta'. Ticotico, alisema katika kuhakikisha klabu yake inajiendesha kisasa ikiwa na ufadhili wa kutosha wameitisha mkutano na wadau wa soka wilayani Kinondoni, ili kujadili na kutoa mawazo yao. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika leo Jumamosi mchana, kwenye majengo ya ofisi ya TANLAP, Kinondoni Biafra. Ticotico aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa klabu ya Red Coast iliyotamba Ligi ya TFF-Kanda, alisema lengo la kuanzisha klabu hiyo ni kuendeleza soka nchini sambamba na kuwasaidia vijana wenye vipaji vya mchezo huo. "Katika kuendeleza soka nchini nimeamua kuanzisha klabu itakayoitwa Golden Bush, ambayo imeshasajiliwa na Jumamosi tunatarajia kufanya mkutano au tuseme kongamano la wadau wa soka kupata mawazo namna ya kuifanya iwe klabu ya kipekee Kinondoni," alisema. Mwisho

No comments:

Post a Comment