STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 6, 2012

Aurora afariki, azikwa Dar atakumbukwa kwa mengi

MDAU wa michezo na burudani hapa nchini, Ally Suleiman 'Aurora' amefariki usiku wa kuamkia juzi na kuzikwa jana kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana ilieleza kwamba Aurora alifikwa na mauti baada ya kuugua kwa muda mrefu na kulazwa kwenye hospital ya Muhimbili. Enzi za uhai wake Aurora aliweza kufadhili mashindano ya urembo, sambamba na michezo mbalimbali ikiwamo ngumi. Miongoni mwa mabondia waliofanikiwa kwa msaada wa Aurora ni bingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Awadh Tamim ambaye alisaidiwa na Aurora kutimiza ndoto hizo. Mbali na Tamim, Aurora aliweza kuisadia timu ya waandishi wa Habari za Michezo nchini 'Taswa FC' katika kufanikisha kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ikiwamo yale ya Media Bonanza yanayofanyika kila mwaka mkoani Arusha. Pia alikuwa akitajwa kama mmoja wa wafadhili wakubwa wa Coastal Union, hivyo kifo chake ni pigo kwa wadau wengi wa michezo na burudani. Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema PEPONI Amiin

No comments:

Post a Comment