STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 1, 2012

Coastal yamng'ang'ania Nsa Job

UONGOZI wa klabu ya Coastal Union ya Tanga, umesisitiza kuwa umeshamalizana na mshambuliaji wa Villa Squad, Nsa Job, aliyedai bado hajasaini kwao. Aidha, uongozi huo umetangaza kuwanasa nyota wengine wawili, Selemain Kassim 'Selembi' aliyekuwa akiichezea African Lyon kwa mkopo akitokea Azam na Mohammed Soud wa Toto Afrika ya Mwanza. Afisa Habari wa Coastal Union, Eddo Kumwembe, aliiambia MICHARAZO kuwa, Nsa aliyenukuliwa hajasaini kokote, ameshamwaga wino kwao tangu wiki iliyopita hivyo ni mali yao kwa ajili ya msimu ujao. Kumwembe alisema, Nsa ni mmoja kati ya wachezaji watatu ambao wameshamalizana nao mpaka sasa kwa ajili ya kusuka kikosi chao kwa msimu ujao, wengine wakiwa ni Selembi. "Nsa ni mmoja wa wachezaji wetu wapya ameshasaini fomu za usajili tangu karibu wiki sasa, tunashangaa akituruka, ila huenda hakupenda watu wajue mapema, lakini ukweli ndio huo msimu ujao ni wetu," alisema. Msemaji huyo aliongeza kuwa mbali na wachezaji hao watatu, pia wanakaribia kumnasa kinda wa timu ya taifa, (Taifa Stars), Simon Msuva aliyekuwa katika timu iliyoshuka daraja ya Moro United akitokea kikosi cha U-20. "Kwa sasa tunamfukuzia Msuva ambapo tunakaribia kumnasa," alisema Kumwembe. Coastal Union iliyorejea Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu na kumaliza katika nafasi ya tano, tayari imetangaza kuwatema wachezaji wake tisa akiwemo Ally Ahmed Shiboli aliyemwaga wino Polisi Moro iliyopanda daraja msimu huu. Wengine waliotemwa sambamba na Shiboli ni Ramadhani Wasso, Ben Mwalala, Samuel Temi, Enock John, Laurent Mugia, Bakari Mohamed, Daudi Changula na Francis Busungu.

No comments:

Post a Comment