STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 1, 2012

Kipa Lyon akiri udhaifu, ajipanga

MLINDA mlango wa kutumainiwa wa timu ya African Lyon, Noel Lucas, amekiri kuwa msimu uliopita timu yao haikuwa katika ubora wake, huku mwenyewe akishuka kiwango jambo lililosababisha timu yao kunusurika kushuka daraja. Hata hivyo, alisema yeye binafsi amekuwa akitumia muda wake wa mapumziko kwao Kigoma kujifua ili kurejesha kiwango chake na akiamini pia usukwaji upya wa kikosi chao unaweza kutoa ushindani mkubwa katika msimu ujao. Akizungumza na MICHARAZO
kwa njia ya simu kutoka Kigoma, Lucas alisema Lyon kwa msimu uliopita ilicheza chini ya kiwango na kusababisha kuwa na wakati mgumu kabla ya kunusurika kushuka daraja dakika za mwisho. Kipa huyo aliyepoteza namba kwa kipa mwenzake Abdul Seif, alisema hata hivyo anashukuru timu yao kupona kurudi Ligi Daraja la Kwanza, akiamini msimu ujao itakuwa timu tishio huku mwenyewe akidai anajipanga upya. "Najipanga kurejesha makali yangu, sio siri msimu uliopita sikuwa katika kiwango kabisa na ndio maana nilipoteza namba," alisema Lucas. Kipa huyo ambaye kabla ya kutua Lyon alitamba timu za Small Boys ya Singida, FC Congo ya Kigoma na Toto Afrika ya Mwanza na mwaka jana kuipa Kombe la Taifa mkoa wa Singida 'Kindai Shooting' kwa mara ya kwanza mkoa huo kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment