STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 2, 2012

Kim Poulsen awaita Bahanunzi, Chuji kikosi cha Stars

MFUMANIA nyavu aliyefunika kwenye michauno ya Kombe la Kagame, Said Bahanunzi wa Yanga na viungo 'watukutu' Athuman Idd Chuji na Ramadhani Chombo 'Redondo' ni kati ya wachezaji 21 waliotangazwa kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa Taifa Stars. Kocha mkuu wa timu hiyo Kim Poulsen amekitangaza kikosi hicho jana kwa ajili ya kujiandaa na pambano la kirafiki la kimataifa linalotarajiwa kuchezwa katikati ya mwezi huu nje ya nchi. Poulsen alisema kikosi hicho kinatarajiwa kuingia kambini wiki ijayo tayari kujiwinda na mechi hiyo ya kirafiki ambayo hata hivyo mpaka sasa haifahamiki itakuwa dhidi ya nchi gani. Kocha huyo alisema amewaita wachezaji hao watatu na wengine kutokana na kuonyesha uwezo mzuri wakati wa michuano ya Kagame, ambapo bahanunzi aliibuka mfungaji bora huku Chuji na Redondo waking'ara katika nafasi ya kiungo mwanzo mwisho. Kim alisema ameomba mechi hiyo ya kirafiki ambayo iko kwenye kalenda ya FIFA ichezwe ugenini kwa lengo la kuwapa uzoefu wachezaji wake. Wachezaji waliotajwa na kocha huyo ni pamoja na makipa watatu, Nahodha Juma Kaseja (Simba), Deogratias Munishi 'Dida'na Mwadini Ally (wote Azam). Mabeki ni nahodha msaidizi, Aggrey Morris na Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba). Viungo walioteuliwa katika timu hiyo ni Chuji na Frank Domayo (Yanga), Haruna Moshi 'Boban', Ramadhani Singano 'Messi' na Mwinyi Kazimito (Simba), Mrisho Ngassa,Redondo na Salum Abubakar 'Sure Boy' (Azam) na Shabani Nditi kutoka Mtibwa Sugar. Wengine ni washambuliaji John Bocco (Azam), Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu(TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo), Bahanunzi na Simon Msuva. Kocha huyo alisema ameshindwa kuwaita Amri Maftah wa Simba na Nurdin Bakari wa Yanga kwa sasa kutokana na kwamba wachezaji hao bado ni majeruhi.

No comments:

Post a Comment