STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 19, 2012

 DEREVA wa treni ya mizingo ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) Ali Kilumanga (57), amefariki dunia huku askari 10 wa jeshi la Polisi nchini wakinusurika kifo kwenye ajali ya treni

Na AFISA HABARI WA TAZARA
DEREVA wa treni ya mizingo ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) Ali Kilumanga (57), amefariki dunia huku  askari 10 wa jeshi la Polisi nchini wakinusurika kifo  kwenye ajali ya treni  iliyotokea karibu na stesheni ya Makambako mkoani Iringa.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TAZARA, Akashambatwa Mbikusita-Lewanika aliwaambia waandIshi wa habari  jijini Dar es Salaam jana kuwa ajali hiyo ilitokea juzi saa 11:40 jioni na kuhusisha Treni No 0755 ya shirika hilo, iliyokuwa ikiokea Dar es salaam kwenda Kapilimposhi  Zambia.
Alitaja chanzo cha ajali hiyo ni hitilafu iliyojitokeza kwenye mfumo wa breki na hivyo kushindwa kufunga breki na baadae kuacha njia na kisha kupunduka, ambapo  dereva wa akiba wa treni hiyo, Mashaka Bujilima alilipata majeraha na kupelekwa Hospitali ya Ilembula iliyopo wilayani Njombe na baadae kuruhusiwa baada ya kupata matibabu.
" Tumepokea kifo cha mpedwa wetu  Kalumanga kwa masikitiko na hazuni kubwa kwa kuwa amekuwa nasi kwa muda mrefu,lakinisasa kametutoka jina la bwana lihimidiwe,’’ alisema Akashambatwa.
Alisema Treni hiyo ilikuwa imebeba shehena ya mizigo mbalimbali ikiwa ni pamoja na injini za teni mbili, magari 16 ya mbolea, magari tisa ya mafuta ya treni na mengine ni magari ya vifaa mbalimbali,ambapo tathimini ya hasara ya mali, inaendelea  kufanyiwa uchunguzi.

"Timu ya wataalamu mbalimbali  na waandamizi, mara moja imenzisha uchunguzi kwa kina sababu ya ajali hii ya  kutisha , lakini ripoti ya awali imewasilishwa kwa serikali  mbili za Tanzania na Zambia," alisema Akashambatwa.

Aidha Akashambatwa, alisema kuwa kwa  huzuni kubwa wametuma  rambirambi zao kwa familia  ya marehemu na  kuwapa  pole kwa niaba ya familia nzima ya TAZARA.
Mwisho

PICHA INAONYESHA JINSI YA MABEHEWA YALIVYOSAMBARATIKA

MABOGI YA BEHWA

BAADHI YA MIZIGO ILIYOSAMBARATIKA

Jengo la shule ya sekondari ya kata ya kiwalani liko katika hali mbaya

Jengo la shule ya sekondari ya kata ya kiwalani liko katika hali mbaya jengo hilo ambalo lina muda wa miaka ipatayo minane toka lijengwe halijaingiwa wanafunzi picha inapnyesha jinsi lilivyo milango imeibiwa silbodi imebomoka kama picha inavyonyesha hivi sasa ndio geto wanafunzi wanaonekana ni wa shule za msingi zilizopo karibu na jengo hilo wakati wanafunzi wanafanya mitihani ya darasa la saba  jee watapelekwa wapi kaama hali ni hii wanafunzi wa darasa la saba shule zilizopo katika kata hiyo ya kiwalani awanafanya mtihani jee wale ambao watakao faulu watakwenda katika shule gani  wanafuzi wanaofaulu katika shule za msingi za kiwalani hupelekwa katika shule za sekondari sehemu za chanika ,mbondole pugu ,kibada shule wananchi wa eneo hilo wanaiomba serikali kufanya kila jitihada wamalize miaka minane toka ijengwe ni mingi.

No comments:

Post a Comment