STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 22, 2012

Minziro amrithi Saintfeit, Mwalusako arejeshwa Jangwani

Lawrance Mwalusako
KLABU ya soka ya Yanga imemrejesha madarakani Katibu Mkuu wao wa zamani, Lawrance Mwalusako na kumpa nafasi kocha msaidizi wa timu hiyo, Fred Felix Minziro kukaimu ukocha mkuu baada ya kumtimua aliyekuwa kocha wake, Tom Saintfiet.
Taarifa zilizopatikana mapema leo leo asubuhi inasema kuwa, Mwalusako atakaimu nafasi ya ukatibu Mkuu iliyokuwa ikishikiliwa na Celestine Mwesigwe,huku Sekilojo Chambua akiteuliwa kuwa meneja wa timu na mtangazaji wa Cloud's, Abdul Mohammed akimrithi Louis Sendeu aliyekuwa amemaliza mkataba wa kuwa Afisa Habari wa Yanga.
Kutokana na mabadiliko hayo leo Yanga itashuka dimba la Taifa kuvaana na JKT Ruvu ikiwa chini ya safu mpya ya benchi lake la ufundi, Minziro akiongoza kama kaimu kocha Mkuu.
Fred Felix Minziro
Yanga haijashinda mechi zake mbili za awali ikianza na suluhu dhidi ya Prisons ya Mbeya kabla ya kubamizwa mabao 3-0 na Mtibwa Sugar.

No comments:

Post a Comment